“Zawadi Ifaayo Mtu Yeyote”
Hayo ndiyo maneno aliyoandika mtu mmoja mwenye umri wa miaka 82 katika Uswisi kuhusu kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Kitabu hicho, kilichotangazwa kwa mara ya kwanza katika 1991, chaeleza katika sura zacho 133 kila tukio katika maisha ya kidunia ya Yesu kama yasimuliwavyo katika zile Gospeli nne. Ni kwa nini msomaji huyo alisisimuliwa hivyo?
“Kitabu hicho chafurahisha kusoma,” yeye akaandika. “Kina chapa zenye kusomeka vizuri na sarufi bora kabisa, jambo ambalo hupati katika vitabu vingine vingi.” Mtu huyo alishangazwa pia na zile picha zaidi ya 200 zenye rangi, ambazo “ni halisi kabisa.” Yeye akaongezea: “Hizo ishara za mwili, ishara za uso, na rangi zenye uanana ni halisi kabisa.”
Mwungwana huyo mzee-mzee apendekeza kwamba watu wawape wengine kitabu hicho kikiwa zawadi. Yeye akiona kuwa “kitabu kizuri sana na chenye kufundisha . . . zawadi ifaayo mtu yeyote.” Nasi twaona vivyo hivyo.
Kama ungependa kuwa na nakala ya Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia nwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
YULE MTU KMUU ZAIDI ALIYEPATA KUISHI