Msaada kwa Wakati Ufaao
Mwanamke mmoja aliandikia ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Australia kuwashukuru kwa kuandaa gazeti Amkeni! juu ya “Kuponya Majeraha ya Kutendwa Vibaya Utotoni.” Yeye aeleza:
“Nikiwa mwenye miaka 12, nilikuwa nikitendwa vibaya kingono na rafiki wa kiume wa mama yangu. Nilijua kwamba yale yaliyokuwa yakitendeka hayakufaa. Hata hivyo, wakati huo nilifikiri nilikuwa nimekuwa mbaya na kufanya jambo fulani la kuchukiza sana na kwamba hiyo ilikuwa njia ya Mungu ya kuniadhibu. Moyo wangu ulikuwa ukivunjika nilipofikiria kumzuru mtu huyo, nikijua vema yale ambayo yangetendeka. Lakini ilinibidi kwenda, kwani mama yangu alimpa ruhusa afanye fantasia zake zilizopotoka kwa kubadilishana na fedha. Mama yangu angewezaje kunifanya hivyo? Nilijifunza kutoonyesha hisiamoyo zangu na kuwa mwenye uchungu kuelekea maisha na Mungu.
“Ilikuwa tu katika 1992 kwamba nilizungumza na mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Nilijifunza mambo mengi. Jambo la maana zaidi lilikuwa kwamba Yehova Mungu hutupenda sisi sote na kwamba hakuwa akiniadhibu.
“Kwa hiyo barua hii ni ya kuwashukuru kwa ajili ya makala zenu za Amkeni! juu ya ‘Majeraha ya Kutendwa Vibaya Utotoni’ katika toleo la Oktoba 8, 1991 [Kiingereza].
“Nimeweka maisha yangu wakfu kwa Yehova na napanga kubatizwa mwaka unaokuja.”
Katika miezi miwili Amkeni! lilipokea barua za shukrani zaidi ya elfu moja kwa ajili ya toleo la Amkeni! lililo juu. Hata hivyo, jambo la maana hata zaidi ya kuonyesha wasomaji jinsi ya kukabili matatizo ya leo, Amkeni! hujenga uhakika katika uandalizi wa Muumba, ukitegemea dhabihu ya fidia ya Yesu, ya ulimwengu mpya wenye amani na usalama utakaoondoa matatizo yote. Ikiwa ungependa kuwa na habari zaidi juu ya huo ulimwengu mpya, au funzo la Biblia nyumbani bila malipo, andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
Awake!
Awake!
Awake!
Children UNDER STRESS How Can They Be Helped?