“Ni Kama Kuitazama Sinema ya Maisha ya Yesu”
Mwanamke mmoja katika Ufaransa alifananisha kusoma kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi na kuitazama sinema kama hiyo. Kitabu hicho chafanya jitihada ya kuzungumzia kila tukio katika maisha ya Yesu ya kidunia yanayozungumziwa katika zile Gospeli. Na kwa kadiri iwezekanavyo, kila ya matukio hayo yameelezwa kwa njia ya utaratibu wa kikronolojia. Mwanamke huyo alielezea:
“Nilipofika mwisho wa kitabu, nilihisi kana kwamba nilikuwa nimekaribishwa na Yesu nishirikiane naye, kuishi kando yake, kushiriki shangwe yake, hisiamoyo zake, kwa ufupi, kila pande ya huduma yake. Vielezi vyenye kuvutia vyaonyesha kikweli hisia na nyutu za wote walioshirikiana na Yesu na hata za Yesu mwenyewe. Kukisoma kitabu hicho kuanzia jalada hadi jalada ni kama kuitazama sinema ya maisha ya Yesu.”
Ikiwa ungependa kupokea nakala ya kitabu hiki chenye jalada gumu cha kurasa 448 au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A. 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo kwenye ukurasa wa 5.
[Picha katika ukurasa wa 32]
YULE MTU MKUU ZAIDI ALIYEPATA KUISHI