“Napendezwa na Kujifunza Mengi Zaidi”
MWANAMUME mmoja wa kutoka Colorado, Marekani, aliandika hayo Desemba uliopita katika barua moja kwa wachapishaji wa gazeti hili. Alieleza hivi:
“Ingawa mimi singeonwa kuwa mtu wa kidini kulingana na viwango vya watu walio wengi, sikuzote nimeamini lazima kuwe kuna mengi yaliyo bora zaidi kuhusu uzima kuliko yale tuonayo na kusikia katika maisha yetu ya siku kwa siku. Sikuzote mimi nimeona wajibu wa kujali mambo ya kiroho, ingawa si kuhusiana na dini fulani hususa.
“Hata hivyo, hivi majuzi nimejikuta katika hali fulani za kusononesha sana nami najikuta bila nguvu ya ndani ya kukabiliana nazo. Matatizo nyumbani na kazini yameongeza wasiwasi wangu kwa kadiri ambayo sijawahi kuwa nayo. . . .
“Ajabu ni kwamba, nilipokuwa nimefikia upeo wa kuvurugika fikira, nilishtukia kupata moja ya fasihi yenu madukani. Maoni yenu kuhusu Baba Mtakatifu yanaburudisha, nami napendezwa na kujifunza mengi zaidi, lakini sina hakika nitapata wapi habari zaidi.
“Ningethamini sana mwongozo wowote mwezao kunipa nijifunze mengi zaidi juu ya Mashahidi wa Yehova na imani zenu. Kama nilivyotaja, niliona ikiwa ajabu kushtukia kupata moja ya fasihi yenu nilipokuwa nimefikia upeo wa kuvurugika fikira—yaweza kuwa ni ishara ya mwongozo wa kimungu.”[1]
Mwanamume huyu alipelekewa nakala ya kitabu kitoacho imani zenye msingi wa Biblia juu ya Mashahidi wa Yehova, chenye kichwa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Ikiwa wewe ungependa kupokea nakala ya kichapo hiki chenye jalada gumu cha kurasa 256 au wataka kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa katika ukurasa 5.