Je! Ulimwengu Huu Utaokoka?
Swali hilo lenye kuvuta fikira ndilo kichwa cha trakti moja inayogawanywa na Mashahidi wa Yehova. Mwaka jana mkazi mmoja wa Washington, D.C., alipokea trakti hii na kusema kwamba udadisi wake uliamshwa. Yeye aliandika hivi:
“Ni wazi kwa mtu anayeishi katika jiji kuu la taifa letu kwamba kwelikweli ulimwengu unafikia mwisho wao. Ireland Kaskazini, ile iliyokuwa Yugoslavia, zile zilizokuwa jamhuri za Muungano wa Sovieti, zote zathibitisha lile giza na mgogoro unaokumba ulimwengu huu leo. Magereza yanayofurika, mweneo mpya wa ugonjwa wa kifua kikuu na kifo cheusi, yote hayo yathibitisha jambo kuu mnalosema katika trakti yenu.”
Mtu huyo aliomba hivi: “Tafadhali nileteeni habari zaidi inayohusu maoni yenu yasiyo na kifani, na lile funzo la Biblia la nyumbani bila malipo mnalotoa.”
Mashahidi wa Yehova huelekeza watu kwa yale ambayo Biblia husema juu ya wakati ujao wa wanadamu. Ikiwa ungependa nakala ya trakti iliyotajwa juu au wataka funzo la Biblia la nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo kwenye ukurasa wa 5.