Fanya Maisha ya Familia Yako Yawe Yenye Furaha
MGONJWA mmoja katika South Carolina, Marekani, alipopeleka trakti Furahia Maisha ya Familia kwa mmoja wa wauguzi, muuguzi huyo alimpigia simu na kumshukuru. Muuguzi huyo alisema kwamba alisoma trakti hiyo pamoja na mume wake na kwamba wote walithamini kuisoma pamoja. Muuguzi huyo alisema hawakuamini kwamba jambo zuri hivyo lilipatikana ili kusaidia familia.
Mgonjwa huyo alieleza hivi: “Muuguzi huyo aliniambia kwamba habari hiyo ilikuwa hasa ile yeye na mume wake wamekuwa wakijadiliana kuhusu mambo yafaayo na yaliyo mazuri ya familia lakini hawakuwa na habari kwamba kulikuwa na jambo lolote kuhusu suala hilo lililochapwa. Yeye alimalizia maneno yake kwenye simu kwa kusema kwamba anabeba trakti hiyo ndogo kokote kule aendako na kuisoma tena na tena. Alisema kwamba kama nina habari nyingine yoyote juu ya maisha ya familia tafadhali nimjulishe.”
Mgonjwa alimpelekea muuguzi kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha naye akafanya mpango wa kukutana na muuguzi huyo ili kukizungumzia. Labda wewe pia waweza kufurahia habari yenye kusaidia kufanya maisha ya familia yako yawe yenye furaha zaidi. Ikiwa ungependa kupokea nakala ya Furahia Maisha ya Familia na Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.