“Kubatilisha ya Wakati Uliopita”
“Twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa.” Hilo lilikuwa kweli wakati maneno haya yalipoandikwa karibu miaka 2,000 iliyopita, na ni kweli leo. Lakini historia, pamoja na kuteseka kwayo kote kwa binadamu, yaweza kubatilishwa?Warumi 8:22.
BROSHUA ya kurasa 32 yenye rangi kamili yenye kichwa Je! Kweli Mungu Anatujali? huzungumzia habari hii hasa. “Mungu atatulipia kuteseka ambako huenda tukawa tulivumilia katika ulimwengu huu,” yasema. “Kwa huruma kuu Mungu atatimiza mengi hata zaidi ya kulipia tu wakati mbaya uliopita tulioletewa.”
Kichapo hicho huleta pamoja ithibati yenye usadikisho kwamba wakati mwangavu ujao watungojea. Baada ya kusoma broshua hii, Mkanada mwenye umri wa miaka 20 aliandika hivi: “Siwezi kueleza kwa maneno jinsi kichapo hiki kilivyogusa moyo wangu sana! Hakika ni kito chenye thamani. Hutukumbusha juu ya tumaini ajabu ambalo Mungu ametuwekea akibani. Nahisi kwamba ile sehemu juu ya ‘Kubatilisha ya Wakati Uliopita’ iliandikwa kwa upendo. Asanteni kwa kutukumbusha jinsi Yehova anatupenda sana.”
Ikiwa ungependa nakala ya broshua hii au ungependa mtu akutembelee nyumbani kwako ili kuzungumzia jambo hili, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani yoyote ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.