Tarehe Usiyopaswa Kusahau
Ile jioni ya kabla ya yeye kufa, Yesu alishiriki kipande cha mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai pamoja na mitume wake na kusema: “Endeleeni kufanya hivi katika kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19, NW.
Mwaka huu mwadhimisho huo ni Ijumaa Aprili 14 baada ya mshuko-jua. Likiwa tokeo la amri ya Yesu, mamilioni ya Mashahidi wa Yehova na watu wenye kupendezwa ulimwenguni pote watakusanyika usiku huu wa pekee kurudia Ukumbusho huu katika njia ambayo Yesu alielekeza. Unakaribishwa kwa uchangamfu mwingi sana ukusanyike pamoja nasi. Tafadhali chunguza kutoka kwa Mashahidi wa Yehova katika mahali penu kwa ajili ya wakati kamili na mahali pa mkutano huo.