“Shukrani kwa Kuwako Kwenu”
Hilo ndilo mwanamume fulani kutoka North Carolina, Marekani aliloandikia makao makuu ya Mashahidi wa Yehova katika Brooklyn, New York. Yeye pia alisema hivi: “Naomba hilo funzo la Biblia nyumbani mnalotoa katika Amkeni! Lakini pia naomba habari ya namna yoyote ambayo mwaweza kuandaa juu ya mada ya helo. . . .
“Nililelewa katika Kanisa Baptisti, lakini hata nikiwa mtoto mdogo, jambo fulani kuhusu mafundisho au desturi zao hazikuwa zenye upatano kwangu.
“Nimekuwa nikisoma vichapo vyenu tangu 1965. Mimi hurejezea Biblia ninaposoma, na kila jambo katika fasihi zenu hulingana na Biblia. Sikuzote nimekuwa nikitaka kujua kweli halisi kuhusu Mungu na Yesu, na naweza kusema kwa moyo mweupe kwamba napata majibu ya kweli kupitia vichapo vyenu na Biblia.”
Labda wewe pia ungethamini habari kuhusu mafundisho ya Mashahidi wa Yehova yenye msingi wa Biblia. Ikiwa ungependa kupata nakala ya trakti Mashahidi wa Yehova Wanaamini Nini? au kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.