“Sitatupa Nakala Zozote Zaidi Hadi Nizisome”
Mwanamume fulani aliandikia watangazaji wa Amkeni! akieleza hivi: “Hivi majuzi nilipata nakala ya Amkeni! ya Aprili 8, 1994, katika mlango-wavu wangu. Ala! Ni nini kimetukia? Mmebuni kichapo kilichofanywa kuwa cha karibuni, chenye kuelimisha cha mwongo huu. Naona badiliko hilo likiwa lenye kushangaza sana, na kwa mara ya kwanza, kwa kweli nilisoma makala hizi. (Kwa kawaida ningefikiri, ‘Ah! walikuwa hapa tena,’ na kulitupa gazeti hilo.) Kulikuwa na jambo fulani katika gazeti hilo kwa kila mtu.”
Kwa kumalizia yeye aliandika hivi: “Mnaendelea katika njia ifaayo. Endeleeni na kazi hiyo nzuri, nami naahidi sitatupa nakala zozote zaidi hadi nizisome.”
Ikiwa ungependa upelekewe nakala ya Amkeni! nyumbani kwako au kutamani funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
Juu: Kwa Hisani ya ROE/Anglo-Australian Observatory, picha iliyopigwa na David Malin