Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 1/8 uku. 32
  • “Kwa Vinywa vya Watoto Wachanga”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Kwa Vinywa vya Watoto Wachanga”
  • Amkeni!—1996
Amkeni!—1996
g96 1/8 uku. 32

“Kwa Vinywa vya Watoto Wachanga”

Mwanamke fulani kutoka Ballito, Natal, Afrika Kusini, alionyesha uthamini mchangamfu kwa ajili ya kitabu Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia kisha akaandika hivi:

“Nina mpwa, Rudi Naidoo, ambaye ana umri wa mwaka mmoja na nusu, naye hutaja majina ya karibu kila mhusika katika hicho kitabu kwa kuona picha tu. Yeye hata hukuambia kile wanachofanya wahusika fulani wa Biblia pichani. Kwa kielelezo, hadithi ya 11 huonyesha Noa akitoa dhabihu. Rudi atueleza, ‘Noa—omba Yehova.’

“Anapoulizwa kile anachofanya Yoshua katika hadithi ya 49, Rudi achukua kikao kama cha Yoshua pichani, huku akisema, ‘Jua simama tuli!’ Yeye hawezi kutamka maneno vizuri lakini husema kwa njia yake mwenyewe yenye kuchekesha, inayopendeza.

“Kwa mara nyingine, nataka kuwashukuru kwa kichapo hiki bora zaidi. Watoto wadogo wanaweza kusimulia kile ambacho watu wazima fulani hawakijui. Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 21:16 kwa hakika ni ya kweli: ‘Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa.’”

Ikiwa ungependa kupata Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia au ungependa mtu akutembelee nyumbani kwako ili kuzungumzia thamani ya elimu ya Biblia nawe, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo kwenye ukurasa 5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki