“Asanteni kwa Kunisaidia Kujifunza Juu ya Yehova!”
Hayo yalikuwa maneno ya kutoka moyoni ya msichana mwenye umri wa miaka 16 kutoka Florida, Marekani. Baada ya kusoma vichapo vinavyotangazwa na Mashahidi wa Yehova, yeye aliandika hivi:
“Siwezi kukumbuka jina lacho, lakini nilisoma kitabu fulani kuhusu maisha ya Yesu ambacho naamini mlikitangaza. Kabla ya kusoma kitabu hicho, nilifikiri nilijua yote niliyohitaji kujua. Naamini katika Mungu na Yesu, mimi husali kabla ya mlo wa jioni na tena usiku, na huishi maisha mazuri ya kiasi. Lakini baada ya kusoma kitabu hicho, niligundua kwamba sijui mengi sana na kwamba nahitaji kuendelea kusoma na kujifunza kumhusu Yehova Mungu na Yesu na wengine katika Biblia.
“Nabadilisha hatua kwa hatua mtindo wangu ili niwe mtumishi mzuri zaidi wa Mungu. Kama si Watch Tower Society, bado ningekuwa simjui Mungu na hadithi zilizo katika Biblia. Asanteni kwa kunisaidia kujifunza kumhusu Yehova!”
Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi ndicho kichwa cha kitabu ambacho huyo msichana alikuwa akirejezea. Ndani yacho jitihada imefanywa ili kutokeza kila tukio la maisha ya kidunia ya Yesu ambalo limewekwa katika zile Gospeli nne. Ikiwa ungependa kupata nakala au ungetaka kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I. B. S. A. Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ifaayo katika ukurasa 5.