Kifaa Muhimu cha Elimu
Mbunge katika nchi ya Sri Lanka alimwandikia “Mhariri wa ‘Amkeni!’” Barua yake inapatikana hapa chini:
“Bwana Mpendwa,
“Lazima isemwe kwamba ingawa gazeti la Amkeni! unalochapisha ni dogo, ni la maana sana na la wakati ufaao. Kila makala moja-moja huwasaidia vijana wa siku hizi kutofautisha waziwazi wema na ubaya.
“Nimesoma makala zote. Maoni yangu ni kwamba kila mwalimu, mwanafunzi, na mzazi kwa kweli apaswa kusoma gazeti hili.
“Nathamini sana kazi ngumu mnayofanya. Nawatakieni mafanikio yenye kuendelea katika kazi yenu.”
Karibu nakala milioni 16 za kila toleo la Amkeni! huchapishwa, katika lugha 78. Ulimwenguni pote gazeti hili huonwa kuwa chombo cha kielimu chenye umaana. Wewe pia waweza kufaidika kwa kulisoma. Ikiwa ungependa nakala au ungependa kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 5.