‘Kila Mtu Duniani Apaswa Kusoma Kichapo Hiki’
MSOMAJI mmoja kutoka Alabama, Marekani, alionyesha uthamini wa moyoni kwa Amkeni! na kuandika:
“Nimemaliza tu kusoma toleo la zamani la gazeti la Amkeni!, lenye kichwa “Washindi Wajapokabiliwa na Kifo.” (Mei 8, 1993) Sikuweza kuacha kulisoma. Lilikuwa lenye kuarifu, lenye mambo ya hakika, lenye kuelimisha.
“Nafikiri kila mtu duniani apaswa kuwa na fursa ya kusoma kichapo hiki!”
Amkeni! linachapishwa katika lugha 78 ili kuelimisha wengine. Makala zalo huzungumza juu ya dini na sayansi, pamoja na masuala ya kijamii, kihisia-moyo, na familia ambayo yamo akilini mwa watu.
Ikiwa ungetaka kupokea Amkeni! au ungetaka mtu akutembelee nyumbani kwako mzungumzie thamani ya elimu ya Biblia, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au anwani ya karibu nawe kwenye ukurasa wa 5.