“Utapata Habari Bora Zaidi Kutoka kwa Amkeni!”
HILO ndilo Pasquale, Shahidi wa Yehova mchanga ambaye alikuwa akichukua kozi fulani katika chuo huko Bari, Italia, aliloambiwa alipomwomba mwalimu wake wa saikolojia habari aliyokuwa nayo kuhusu uraibu wa dawa za kulevya. Hata hivyo, wakati uliopita mwalimu huyu alikuwa ameonyesha ubaguzi kuelekea Mashahidi wa Yehova. Ni nini kilichosababisha mtazamo wake ubadilike?
Pasquale alieleza hivi: “Mwishoni mwa somo moja, mwalimu huyo aliomba wanafunzi wake msaada katika kupata habari juu ya kutendwa vibaya kwa watoto, habari aliyokuwa akitayarisha kuwa tasnifu ya baada ya kuhitimu. Nilikumbuka matoleo machache ya Amkeni! ambayo yalishughulikia habari hii na habari inayohusiana nayo, kama vile ‘Mafunzo ya Ngono—Ni Nani Anapaswa Kuyafunza?’ (Oktoba 8, 1992). Hata hivyo, nikijua ubaguzi wa mwalimu wangu kuelekea Mashahidi, nilimwomba mwanadarasa mwenzangu ampe magazeti hayo.”
Pasquale afafanua kile kilichotokea wakati, siku chache baadaye, alimwomba mwalimu wake maandishi fulani aliyotaka juu ya habari ya uraibu wa dawa za kulevya: “Yeye hakujibu mara hiyo. Badala ya hivyo, alisimama na kuja kunisalimu kwa mkono. Alisema kwamba hakuwa ametaka kukubali magazeti ya Mashahidi wa Yehova mbeleni kwa sababu aliyaona kuwa yasiyo na ujuzi na ya kitoto. Ingawa hivyo, baada ya kuyasoma alibadili maoni yake. Alisema kwamba alipata mambo yaliyokuwa katika magazeti hayo kuwa yenye msaada sana kulingana na maoni ya kijamii. Alisema kwamba atatia ndani hoja kutoka Amkeni! katika tasnifu yake.”
Namna gani ombi la Pasquale la maandishi juu ya uraibu wa dawa za kulevya? “Nitakupatia kwa utayari kabisa,” aliitikia, “lakini utapata habari bora zaidi kutoka kwa Amkeni! Hilo ni gazeti ambalo hushughulika na habari zifaazo, nalo ni lenye msaada, hata kwenye kiwango cha chuo kikuu.”
Amkeni! huzungumzia matatizo ya wakati huu nalo hujitahidi kutoa msaada wenye kutumika kwa wale wanaokabili magumu madogo au makubwa katika maisha ya kila siku. Ikiwa ungependa kujua msaada ambao Biblia yaweza kuandaa, wasiliana na Mashahidi wa Yehova, ambao hueneza Amkeni!, au uandikie anwani ihusuyo kati ya zilizoorodheshwa kwenye ukurasa 5.