Yale “Makosa Saba ya Ulimwengu”
INASEMEKANA kwamba Mohandas Gandhi alitayarisha orodha ya yale aliyoyaita “Makosa Saba ya Ulimwengu.” Hayo ni:
• Mali bila kazi
• Raha bila dhamiri
• Ujuzi bila utu
• Biashara bila maadili
• Sayansi bila ubinadamu
• Ibada bila dhabihu
• Siasa bila kanuni
Inasemekana kwamba mjukuu wake Arun Gandhi aliongeza la nane:
• Haki bila madaraka
Labda unaweza kudokeza mengine machache, lakini orodha hii kwa kweli inafanya tufikirie kwa uzito. Suluhisho la Biblia kwa “makosa” hayo limejumlishwa katika amri mbili: “‘Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’ Hii ndiyo amri kubwa zaidi sana na ya kwanza. Ya pili, kama hiyo, ni hii, ‘Lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Juu ya amri mbili hizi Sheria yote yaning’inia, na Manabii.”—Mathayo 22:37-40.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 20]
UPI/Corbis-Bettmann