‘Utumishi Mkubwa kwa Wanadamu’
“Mmetolea wanadamu utumishi mkubwa kwa kuchapisha kitabu hiki. Ni cha kiajabu. Ni mkusanyo bora zaidi. Chastahili kuonyeshwa uthamini.
“Uzuri wa kitabu hicho ni kwamba hushughulika na kila sehemu ya dini, na katika kufanya hivyo uangalifu ulitolewa kutochambua. Mmekusanya kitabu kizuri sana. Kitabu cha kipekee.”
Msomi huyo mwenye digrii za juu atokaye Tiruchchirappalli, India, aliyeandika barua hii, alikuwa akirejezea kitabu gani? Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, mkusanyo wenye kurasa 384 wa vyanzo na mafundisho ya dini kuu za ulimwengu—Dini ya Hindu, Dini ya Buddha, Dini ya Tao, Dini ya Confucius, Dini ya Shinto, Dini ya Kiyahudi, Ukristo, na Uislamu. Sura za mwisho hueleza ukosefu wa itikadi wa siku ya kisasa na kumrudia Mungu wa kweli. Zaidi ya nakala milioni 16 za kitabu hiki zimepigwa chapa katika lugha 37.
Msomi huyo alikuwa amesoma nakala iliyoazimwa. Alitaka yake binafsi. Ikiwa ungetaka kujichunguzia kitabu hiki kilicho na picha, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova katika eneo lako au uandike kwa kutumia anwani iliyo karibu kwenye ukurasa 5 wa gazeti hili.