Ni Nini Unachojua Kumhusu Yesu?
Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 84 anayeishi Marekani alisema hivi kuhusu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, kitabu chenye picha cha kurasa 448 kuhusu maisha ya Yesu Kristo: “Nimeisoma Biblia kabisa mara kadhaa, na kitabu Mtu Mkuu Zaidi kimenisaidia kufahamu vizuri zaidi usomaji wangu wa Biblia.” Kitabu hicho hufanya masimulizi ya Biblia ya maisha ya Yesu yawe yenye kupendeza na yenye uhalisi kwake.
“Mimi sichoki kukisoma kitabu hicho,” akaandika. “Nimekisoma mara saba na nimeanza kukisoma tena. Moyo wangu huguswa na sifa nzuri ajabu za Yesu. Nisomapo sura kuhusu juma la mwisho la Yesu duniani, napatwa na maumivu kwa jinsi alivyotendwa vibaya, hasa saa zake za mwisho-mwisho, na kwa kifo chake kwenye mti wa mateso. Hata hivyo, yeye alimtukuza Baba yetu wa kimbingu, Yehova.”
Katika kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, jitihada imefanywa ili kutokeza kila tukio katika maisha ya Yesu ya kidunia ambalo hutajwa katika zile Gospeli nne. Chaweza kukusaidia ujifunze mengi zaidi kuhusu Yesu. Ikiwa ungependa kupata nakala au ungependa funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., P. O. Box 47788, Nairobi, Kenya, au kwa kutumia anwani ihusuyo kwenye ukurasa 5.