Usiku wa Kukumbuka
JUMAPILI, MACHI 23, 1997
USIKU kabla ya kufa kwake, Yesu Kristo alianzisha pamoja na mitume wake Ukumbusho wa kifo chake. Kwenye mlo sahili ambao katika huo alitumia divai na mkate usiotiwa chachu vikiwa mifano, Yesu aliamuru hivi: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.”—Luka 22:19.
Mashahidi wa Yehova wanakukaribisha kwa uchangamfu ushiriki pamoja nao katika kukumbuka Ukumbusho huu wa kila mwaka. Mwaka huu Ukumbusho huo utafanywa baada ya jua kushuka, Jumapili, Machi 23, tarehe inayolingana na Nisani 14 kwenye kalenda-mwezi ya Biblia. Tafadhali pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu juu ya mahali barabara pa kukutania na wakati.