Maswali Yake Yote Yajibiwa
Mtu fulani ambaye alipatikana na Mashahidi wa Yehova katika India alipata kwamba yale waliyofundisha yalikuwa tofauti sana na yale aliyokuwa amefundishwa kanisani. Alizungumza na Mashahidi wa Yehova kuhusu jambo hilo na hata akaandika barua kwenye ofisi yao ya tawi katika India ili kuuliza maswali.
Kisha, siku moja mtu huyo aliandika barua ambayo ilianza kwa kusema hivi: “Ndugu zangu wapendwa sana mlio Lonavla”—ambapo ni mahali pa ofisi ya tawi ya Mashahidi katika India. Yeye alieleza: “Shaka zangu zote na maswali yangu yote yalijibiwa yenyewe katika gazeti la Amkeni! la Mei, 8, 1995, chini ya kichwa ‘Je! Umepata Kujiuliza?’ Nimesadiki kabisa kwamba Mashahidi wa Yehova wana kweli.”
Makala hiyo katika Amkeni! ilijibu maswali kama haya yafuatayo: “Je, ibada ya kweli ingejaribu kuficha au kuondoa jina la Mungu lililofunuliwa?” “Ni mwenendo wa aina gani ambao dini ya kweli yapaswa kutokeza kama tokeo la mafundisho yayo?” “Je ibada inayokubalika na Mungu ingeshiriki katika vita na mauaji ya kijamii au ya kikabila?”
Tuna hakika kwamba Amkeni! laweza pia kukusaidia katika utafutaji wako wa kweli ya Biblia. Ikiwa ungependa kupokea nakala au ikiwa ungependa mtu fulani akutembelee nyumbani ili kujadili nawe Biblia, tafadhali andikia I.B.S.A., P. O. Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.