“Walisisimuka Kama Watoto”
Hivyo ndivyo Sergei, baba ya watoto watatu mwenye umri wa miaka 32, alivyoeleza itikio la rafiki zake alipowaonyesha kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Sergei, ambaye huishi Tatarstan, Urusi, aeleza kilichotukia:
“Kwanza tuliangalia picha na kusoma maelezo ya picha. Mazungumzo ya kindani yakafuata. Rafiki zangu wote ni akina baba na mama wachanga . . . Sote huhudhuria kanisa wakati wa Ista na wakati wa ubatizo, lakini hatukuhusika na kanisa zaidi ya hapo.
“Kwa upande ule mwingine, tunapendezwa kama nini na fasihi yenu! Jalada maridadi lenye rangi nzuri la kitabu lanasa uangalifu upesi. Ukianza kukisoma, ni vigumu kukiacha. Wataka kushiriki na majirani mambo ambayo umejifunza. Isitoshe, wahisi umetosheka na kuridhika baada ya kusoma na kuizungumza habari hiyo. Hatimaye, tumepata jambo lenye kufurahisha, la akili, na lenye manufaa la kuzungumzia.
“Bila shaka, twaishi katika hali ya utupu wa kiroho. Kila mtu azungumza kuhusu pesa, matatizo, wasiwasi, na njama. Mambo haya huangamiza tu moyo kabisa. Baada ya kuyafikiria, huwezi kupata usingizi mara moja, na asubuhi hutaki kuamka na kukabiliwa na matatizo chungu nzima yasiyopendeza ya kibinadamu.”
Huenda ukawa na hisia kama hizo na ungefurahia kuwa na nakala ya kichapo hiki chenye kuvutia kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, tengenezo la kimataifa lenye wanafunzi wa Biblia zaidi ya milioni tano. Ikiwa ungependa habari zaidi au funzo la Biblia nyumbani bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.