Jambo Ambalo Trakti za Biblia Zaweza Kutimiza
Katika jiji la Golitsino, karibu na Moscow, Urusi, mmoja wa Mashahidi wa Yehova alimpa mwanamke mmoja aliyekuwa akimsukuma mtoto kwenye kigari, ile trakti Furahia Maisha ya Familia. Shahidi huyo aliendelea kutembea, lakini punde tu akasikia sauti ya yule mwanamke akimwita kupata uangalifu wake. Alikuwa akikimbia amfikie, akiwa angali anasukuma mtoto wake katika kigari.
Huyo mwanamke alisema kuwa alipendezwa kujifunza zaidi, kwa hiyo huyo Shahidi akampa trakti mbili zaidi zenye vichwa vya Biblia. Alimpa pia nambari yake ya simu ili awasiliane naye baadaye. Mwanamke huyo alimpigia simu jioni hiyohiyo na mipango ikafanywa ili awe na funzo la Biblia nyumbani kila juma. Katika miezi saba tu, mwanamke huyo na dada yake walijitoa wakfu ili wamtumikie Mungu nao wakabatizwa.
Ikiwa ungependa kusoma trakti za Biblia zenye vichwa Furahia Maisha ya Familia, Faraja kwa Walioshuka Moyo, Ni Nani Hasa Anayeutawala Ulimwengu?, na Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani iliyo karibu zaidi nawe iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.