“Mnatolea Watu Utumishi Ulio Bora”
Mwanamume kutoka Goa, India, alipokea nakala mbili za Amkeni! kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wawili waliomtembelea nyumbani mwake. Baada ya kuyasoma, aliandika barua ifuatayo kwa wachapishaji wa gazeti hilo:
“Ninawashukuru sana wale bibi wawili waliotembelea makao yangu siku iliyopita na kuacha nakala za gazeti Amkeni! Nikifikiri hayo yalikuwa propaganda, sikuyakazia uangalifu kwa muda fulani. Lakini siku moja nilitupia jicho mojawapo ya hayo magazeti, juu ya ‘Msitu wa Mvua wa Amazon’ (Machi 22, 1997). Nilianza kulisoma na singeweza kuliweka kando mpaka nilipolisoma lote na kwa uangalifu.
“Nilipata habari katika Amkeni! kuwa yenye kupendeza na yenye kuarifu. Ule unamna-namna wa habari pia ulinivutia. Lile lililonipendeza zaidi lilikuwa ule mfikio wa busara na wenye usawaziko sana wa makala mbalimbali.”
Huyu msomaji wa mara ya kwanza wa Amkeni! aliongezea: “Mnatolea watu huduma bora kwa kuwaletea habari ya thamani jinsi hii nyumbani kwao.”
Wewe pia waweza kufaidika kwa kusoma Amkeni! Ikiwa ungependa kupokea nakala nyingine au ikiwa ungependa mtu fulani akutembelee nyumbani ili kuzungumza juu ya Biblia pamoja nawe, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5.