Aprili 11, 1998—Siku ya Kukumbuka
Jioni kabla ya kufa kwake, Yesu alipitisha mkate usiotiwa chachu na kikombe cha divai kwa mitume wake na kuwaagiza wale na kunywa. Pia aliwaambia: “Fulizeni kufanya hili katika ukumbuko wangu.”—Luka 22:19.
Mwaka huu siku ya ukumbusho ya sherehe hii itakuwa Jumamosi, Aprili 11, baada ya jua kushuka. Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote watakusanyika usiku huu wa pekee kusherehekea Ukumbusho huu katika njia ambayo Yesu aliamuru. Unaalikwa kwa uchangamfu mwingi kujiunga nasi ukiwa mtazamaji. Tafadhali pata habari kutoka kwa Mashahidi wa Yehova wa kwenu juu ya wakati barabara na mahali pa kukutania.