Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 6/8 kur. 12-24
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Amkeni!—1998
  • Vichwa vidogo
  • Majibu ya Maswali
Amkeni!—1998
g98 6/8 kur. 12-24

Je, Wajua?

(Majibu ya maswali haya yaweza kupatikana katika maandiko ya Biblia ambayo yameonyeshwa, na orodha kamili ya majibu imechapwa kwenye ukurasa wa 24. Kwa habari zaidi, ona kichapo “Insight on the Scriptures,” kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.)

1. Ni nani ‘waliopiga kelele kwa furaha’ Mungu ‘alipoweka jiwe la pembeni’ la dunia? (Ayubu 38:4-7)

2. Ufalme wa Mungu hautapatwa na nini kamwe? (Danieli 2:44)

3. Daudi alijilinganisha na nini ili kumwonyesha Sauli kwamba hakukuwa na haja yoyote ya Sauli kumwinda? (1 Samweli 24:14)

4. Malaika wa saba alimwaga bakuli lake la hasira ya Mungu juu ya nini? (Ufunuo 16:17)

5. Kwa nini wazao wa Yakobo wanaitwa Waisraeli? (Mwanzo 32:28)

6. Ni maji gani yenye chumvi nyingi zaidi duniani? (Ona Mwanzo 14:3.)

7. Kwa nini Wakristo wanahimizwa kusali “kuhusu wafalme na wote wale walio katika cheo cha juu”? (1 Timotheo 2:1, 2)

8. Ni usemi gani wa Kisemiti ambao Yesu aliutumia alipokuwa akimponya mwanamume kiziwi aliyekuwa na kizuizi cha usemi? (Marko 7:34)

9. Yesu alifanyia wapi muujiza wake wa kwanza? (Yohana 2:11)

10. Jina la pili alilopewa Esau lilikuwa jipi? (Mwanzo 36:1)

11. Yesu alitumia mnyama gani katika kielezi ili kuonyesha tamaa yake ya kukusanya Yerusalemu lisiloitikia? (Luka 13:34)

12. Ni metali gani itumiwayo kunoa vifaa vya metali iyo hiyo? (Mithali 27:17)

13. Katika njozi, Yohana alimwona Mwana-Kondoo na wale 144,000 wakiwa wamesimama wapi? (Ufunuo 14:1)

14. Ni nani aliyepelekea baraza linaloongoza katika Yerusalemu lile swali muhimu la kutahiriwa kwa wasio Wayahudi? (Matendo 15:2)

15. Jiji kuu la ufalme wa kaskazini wa makabila kumi ya Israeli lilikuwa gani? (1 Wafalme 16:29)

16. Nambari ya “hayawani-mwitu” ni gani? (Ufunuo 13:18)

17. Kwa nini malkia wa Sheba alisafiri kwenda Yerusalemu? (1 Wafalme 10:4)

18. Ni mfalme yupi wa Yudea aliyekuwa na bidii sana kwa ajili ya ibada safi hivi kwamba alimwondoa nyanya yake katika wadhifa wake kwa sababu alifanyiza “sanamu ya kuchukiza”? (1 Wafalme 15:13)

19. Malaika wa pili alimwaga bakuli lake la hasira ya Mungu ndani ya nini? (Ufunuo 16:3)

20. Ni nani aliyekuwa mfalme mwovu wa Israeli aliyemtendea vibaya Tifsa? (2 Wafalme 15:16)

21. Ni silaha gani iliyotupwa kwa ukawaida? (Yoshua 8:18)

22. Mwezi wa Ethanimu baada ya uhamisho wa Babiloni uliitwaje?

Majibu ya Maswali

1. Wana wa kimalaika wa Mungu

2. “Hautaangamizwa”

3. “Kiroboto”

4. Hewa

5. Kwa sababu Mungu alibadili jina lake liwe Israeli

6. Bahari ya Chumvi

7. “Ili tupate kuendelea kuishi maisha yaliyo shwari na matulivu”

8. Efatha (linalomaanisha “funguka”)

9. Kana

10. Edomu

11. Kuku

12. Chuma

13. Kwenye Mlima Zayoni wa kimbingu

14. Paulo na Barnaba

15. Samaria

16. 666

17. Ili kusikia hekima ya Solomoni

18. Asa

19. Bahari

20. Menahemu

21. Mkuki

22. Tishri

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki