Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 10/8 kur. 20-27
  • Je, Wajua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Wajua?
  • Amkeni!—1998
  • Vichwa vidogo
  • Majibu ya Maswali
Amkeni!—1998
g98 10/8 kur. 20-27

Je, Wajua?

(Majibu ya maswali haya yaweza kupatikana katika maandiko ya Biblia ambayo yameonyeshwa, na orodha kamili ya majibu imechapwa kwenye ukurasa wa 27. Kwa habari zaidi, ona kichapo “Insight on the Scriptures,” kilichochapishwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.)

1. Bahari ya Galilaya iliitwaje pia, jina linalotokana na jiji lililo magharibi mwa ukingo wake? (Yohana 6:1; 21:1)

2. Ni wapi waliposimama wapiganaji wa Daudi 200 kati ya 600 kwa sababu ya kuishiwa nguvu walipokuwa wakiwafuata Waamaleki waliokuwa wamewateka wake wawili wa Daudi? (1 Samweli 30:9, 10)

3. Rahabu alitumia nini kuwaficha wapelelezi wawili wa Israeli? (Yoshua 2:6)

4. Ni nini ambacho Paulo alisema kingewasaidia Wakristo ili ‘waweze kumtolea Mungu katika njia ya kukubalika utumishi mtakatifu’? (Waebrania 12:28)

5. Kulingana na Sheria ya Kimusa, bwana-mkubwa alipaswa kufanya nini ikiwa mtumwa wake hakutaka kuwekwa huru? (Kutoka 21:6)

6. Ni jiji lipi la Edomu lililojulikana kwa hekima yake? (Yeremia 49:7)

7. Milango ya Patakatifu Zaidi pa hekalu la Solomoni ilijengwa kwa mbao zipi? (1 Wafalme 6:31-33)

8. Kulingana na Mithali 6:17-19, ni mambo gani saba anayoyachukia Yehova?

9. Herufi ya mwisho ya alfabeti ya Kiebrania ni ipi? (Zaburi 119:169, NW, maandishi ya utangulizi)

10. Ni nini ambacho Paulo alisema kitatukia kwa wale wanaopanda kwa uhaba, kwa kulinganishwa na wale wanaopanda kwa wingi? (2 Wakorintho 9:6)

11. Alipokuwa akidai kwamba Yehova aondoe baraka zake kutoka kwa Yobu, Shetani alidai Yobu angefanya nini? (Ayubu 1:11)

12. Ni nini kitakacholipata “jina la mtu mwovu”? (Mithali 10:7)

13. Yesu alipowasafisha watu kumi wenye ukoma, ni wangapi kati yao waliokosa kuonyesha shukrani? (Luka 17:17)

14. Waisraeli walifanya nini ndipo kuta za Yeriko zikaanguka? (Yoshua 6:5)

15. Ni vizuizi vipi vilivyowekewa Waisraeli waliotukia kuona kiota cha ndege? (Kumbukumbu la Torati 22:6, 7)

16. Kwa nini Yehova aliwapa Waisraeli pendeleo la pekee? (Isaya 41:8)

17. Ni maakida wangapi waliokuwa washauri wa Mfalme Ahasuero, wakishirikiana katika hukumu dhidi ya Malkia Vashti? (Esta 1:14)

18. Sadaka iliyotolewa kwa Yehova ambayo hakuna sehemu yoyote iliyobakishwa na mwabudu. (Mambo ya Walawi 1:4)

19. Ni mambo gani mawili aliyosema Paulo ambayo mtu apaswa afanye ili aokolewe? (Waroma 10:9)

20. Ilimchukua Solomoni muda gani hivi kulijenga hekalu? (1 Wafalme 6:1, 38)

21. Ni nini kilichofanywa katika siku za zamani ili kummaliza nguvu adui aliyetekwa? (Waamuzi 1:6)

22. Musa aliweka wapi mbao za mawe ya Sheria mara ya kwanza? (Kumbukumbu la Torati 10:1-5)

23. Ni kitabu kipi cha Biblia kinachoeleza kwa msingi utendaji wa Petro na Paulo?

24. Aliitwaje yule msichana-mtumishi, aliyefurahi sana kwa kusikia sauti yake, na aliyekimbia kuwaeleza wengine kwamba Petro alikuwa mlangoni, bila kumfungulia? (Matendo 12:13, 14)

Majibu ya Maswali

1. Bahari ya Tiberiasi

2. Kijito Besori

3. Mabua ya kitani

4. “Hofu ya Kimungu na kicho”

5. ‘Kulitoboa sikio lake kwa uma’

6. Temani

7. Mbao za Mzeituni

8. “Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; moyo uwazao mawazo mabaya; miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; shahidi wa uongo asemaye uongo; naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu”

9. Taw

10. Wanavuna kulingana na jinsi walivyopanda

11. Angemkufuru Yehova mbele za uso wake

12. Litaoza

13. Tisa

14. Walipopiga kelele

15. Wangeweza kutwaa makinda lakini, koo alipaswa kuachwa

16. Walikuwa “mzao [“mbegu,” NW] wa Ibrahimu,” rafiki ya Yehova

17. Saba

18. Sadaka ya kuteketezwa

19. Mtu apaswa kutangaza hadharani kwamba Yesu ni Bwana, na kudhihirisha imani kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu

20. Miaka saba

21. Vyanda vyake vya mikono na vya miguu vilikatwa

22. Ndani ya sanduku lililotengenezwa kwa mshita

23. Matendo

24. Roda

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki