Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 6/8 uku. 31
  • ‘Kazi Yako Hunufaishaje Jumuiya?’

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • ‘Kazi Yako Hunufaishaje Jumuiya?’
  • Amkeni!—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Kushangilia Mavuno Katika India
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Imani ya Familia Yajaribiwa
    Amkeni!—2004
  • Twatambuliwa kwa Mwenendo Wetu
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 6/8 uku. 31

‘Kazi Yako Hunufaishaje Jumuiya?’

SWALI hilo lilizushwa na Chandrakant Patel, mwandishi wa habari wa India, kwa mshiriki mmoja kwenye makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova, katika Brooklyn, New York. Bw. Patel alikuwa amekuja kuzuru makao hayo na alivutiwa sana na yale aliyoona na kusikia hivi kwamba aliporudi India, aliandika makala kwa niaba ya gazeti la habari la lugha ya Gujarati.

Akitofautisha itikadi fulani za Mashahidi wa Yehova na zile za mashirika ya kanisa huko India, Bw. Patel aliandika kwamba Mashahidi wa Yehova huamini Mungu mweza yote, Yehova, kinyume na fundisho la Utatu ambalo hufundishwa makanisani kwa kawaida na kwamba hawatumii mifano katika ibada yao. Alisema kwamba Mashahidi wa Yehova wana kanuni za juu kwa sababu wanashikilia kwa dhati maadili ya Kikristo yanayoonyeshwa katika Biblia kuhusu uzinzi, utoaji-mimba, na kuchukia au kuua binadamu-mwenzi. Aliwafafanua Mashahidi kuwa watu wenye kuamanika, wenye upendo, wastahimilivu, na wenye kuchangia hali njema ya wenzao na vilevile wasioogopa na wenye bidii katika kueneza ujumbe wa Biblia kwa wengine.

Mwandishi wa habari kutoka India alipata jibu gani kwa swali lake, ‘Kazi yako hunufaishaje jumuiya?’ Aliandika: ‘Jibu lilikuwa, elimu ya Biblia ni yenye manufaa katika nyanja zote za maisha.’ Bw. Patel alitaka kujua hasa kuhusu nyanja za kitaaluma za utunzaji wa afya na kazi ya kuajiriwa. Akitaja sehemu za ufafanuzi aliopewa, aliripoti hivi: ‘Mtu akifuata shauri la Kimaandiko la kujiepusha na vitu vyenye kudhuru kama vile tumbaku na dawa za kulevya na kuishi maisha safi, anaweza kuepuka maradhi ya namna mbalimbali. Na watu wenye kufanya kazi kwa bidii, wenye maisha safi, na wanyoofu wanaweza kuajiriwa kazi kwa urahisi. Isitoshe, kusuluhisha matatizo kwa njia yenye fadhili na ya upendo hutokeza uhusiano wenye amani pamoja na wengine. Hivyo kufundisha watu yale ambayo Biblia husema hunufaisha jumuiya.’

Mwandishi huyu wa habari alijionea mwenyewe mafundisho ya Biblia yakifanya kazi kwenye makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova. Makala yake ilisifu usafi na uchangamfu wa wafanyakazi wa kujitolea kwenye kitovu hicho cha utendaji wa kiroho. Wewe pia unaweza kunufaika na mafundisho ya Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukuonyesha jinsi ya kufanya.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

Mandharinyuma ya gazeti la habari: Courtesy Naya padkar, Gujarati Daily published from Anand, India

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki