Ilimtia Moyo Kuisoma Biblia Tena
Hivyo ndivyo broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote ilivyomfanya mwanamume mmoja kutoka Mexico. Hivi ndivyo alivyoandika kuhusu broshua hiyo:
“Njia mpya na yenye akili ambayo habari hiyo yazungumziwa humwacha msomaji awe na tamaa ya kusoma Biblia. . . . Mimi binafsi nilifurahia utangulizi, marejezo, na habari zenye kichwa ‘Kitabu “Kisemacho” Lugha Zilizo Hai,’ ‘Je, Kitabu Hiki Chaweza Kutumainiwa?,’ na ‘Je, Kitabu Hiki Chaafikiana na Sayansi?’ Kila moja ni sahili, yenye msingi unaofaa, na kutolewa kielezi. . . .
“Mimi mwenyewe, nimetiwa moyo sana na habari hii. Nimekuwa na shangwe ya kusoma Biblia yote nzima, lakini jambo nililofanya kwanza baada ya kusoma broshua hii lilikuwa kupata Biblia yenye chapa kubwa. Sasa, juma moja limepita, ninasoma Biblia kwa uchangamfu mwingi sana na tamaa ya kujifunza mengi zaidi.”
Tuna uhakika kwamba wewe pia utanufaika zaidi na usomaji wa broshua hii nzuri yenye kurasa 32, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote. Waweza kupokea nakala moja kwa kujaza na kupeleka kuponi inayoandamana hapa kwenye anwani inayoonyeshwa kwenye kuponi au kwenye anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote.
□ Tafadhali tumeni mtu awasiliane nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
The Trustees of the Chester Beatty Library, Dublin