Kichapo Chenye Kusudi
MENEJA wa maktaba ya umma huko Prague, Jamhuri ya Cheki, aliweka uchanganuzi wa kurasa mbili juu ya gazeti Amkeni! kwenye ubao wa habari katika maktaba. Miongoni mwa mambo aliyoandika ni yale yafuatayo:
“Mimi si mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Mimi si mtegemezaji aliyejitoa wala mpinzani mkali wa Watch Tower Society. Hata hivyo, sina budi kupendekeza kwa uchangamfu gazeti Amkeni!, ambalo nimekuwa nikilisoma kwa muda fulani. Kusoma kichwa chake tu mara moja kwa siku kwaweza kukufaidi sana. Hata hivyo, si kichwa tu pekee bali yaliyomo ndani ya gazeti hilo ni nyongeza nzuri kwa magazeti ya kibiashara . . .
“Amkeni! lina dhana iliyofikiriwa vizuri. Huwa na makala zenye habari ambazo magazeti yale mengine husita kuchapisha kwa sababu mbalimbali. Hutoa vidokezi, huelimisha watu tufeni pote . . . Amkeni! halihukumu. Hutoa mambo ya hakika na maoni ya wenye mamlaka, huonyesha matokeo ya pande zote hasi na chanya, hukabili matatizo ya sasa kwa manukuu ya Biblia, nalo humwacha msomaji ajiamulie mwenyewe. Isitoshe, Amkeni! huuliza—na kufundisha wasomaji waulize—maswali.”
Katika ukurasa wa 4 wa kila gazeti, sehemu “Sababu ya Amkeni! Kuchapishwa” yaeleza: “La maana kuliko yote, gazeti hili hujenga uhakika katika ahadi ya Muumba ya kuleta ulimwengu mpya wenye amani na usalama ambao uko karibu kuchukua mahali pa mfumo wa mambo uliopo mwovu na usiotii sheria.”
Utaona ahadi hii ya Mungu ikizungumziwa katika sehemu mbili za mwisho za broshua yenye kurasa 32 yenye kichwa Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje? Sehemu hizi zina kichwa “Karibuni Kusudi la Mungu Kutimizwa” na “Ishi Milele Juu ya Dunia-Paradiso.” Unaweza kupokea broshua hii kwa kujaza na kupeleka kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa kwenye kuponi au kwa anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni nakala ya broshua Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.