‘Hutokeza Tamaa ya Kujua Mengi Zaidi’
MSOMAJI kutoka North Carolina, Marekani, aliandika yaliyo juu kuhusu kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? kilichochapishwa mwaka jana. Aliongeza kusema hivi: “Asanteni kwa kuchochea tamaa ya kutaka kujua moyoni na akilini mwangu.” Kisha akaandika yafuatayo:
“Leo, nilipokuwa nimeketi kwenye baraza langu la nyuma, nilimwona kiwavi mwenye rangi ya kijani changavu. Alitembea-tembea kwa uangalifu sana. Kwa tahadhari, alihakikisha kila hatua aliyopiga mbele ilikuwa salama, kisha kwa madaha, akaendelea. Hata hivyo, alikuwa kwenye ubao wa mwisho wa baraza letu. Nilifikiri kwamba kama angeanguka kwa sababu fulani —labda kuanguka kutoka meta moja na nusu—labda hangeumia vibaya. Lakini, kama mwanadamu angeanguka umbali unaolingana na huo, kwa kweli angekufa.”
Mwanamke huyo alijiuliza, “Ni nini ambacho humfanya kiwavi huyo mdogo mwenye rangi ya kijani kuwa tofauti sana?” Alikata kauli kwamba hilo ni “mojawapo tu ya mamilioni ya maswali ambayo itasisimua yakijibiwa. Lakini, kwa wakati huu, twaweza kujifunza mambo mengi kuhusu Muumba wetu kutokana na kiwavi huyo mdogo wa rangi ya kijani.”
Utaona likiwa jambo lenye kuelewesha jinsi ambavyo kusoma juu ya ulimwengu wetu wa ajabu, na vilevile unamna-namna wa viumbe tata duniani, huandaa uthibitisho wa kuwapo kwa Muumba Mtukufu. Unaweza kupata nakala ya kitabu hiki chenye jalada nyepesi chenye kurasa 192, kwa kujaza kuponi iliyo hapa na kuipeleka kwenye anwani inayoonyeshwa kwenye kuponi au anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni nakala ya kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali?
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila malipo.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 32]
J. Hester and P. Scowen (AZ State Univ.), NASA