Picha Ambayo Hangeweza Kuisahau
KAREN, ambaye amekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova kwa zaidi ya miongo miwili, aligundua kwamba baba yake hakupendezwa kamwe kuzungumza naye juu ya dini. Ingawa hivyo, mambo yalibadilika hivi majuzi. Alikuwa amelazwa hospitalini, akipata nafuu baada ya upasuaji. Siku moja alisoma gazeti lote la habari kwa sababu ya uchoshi mwingi. Alishtuka. Baadaye, baada ya kurejea nyumbani, alimwita bintiye. Karen aeleza: “Baba aliniambia hivi kupitia simu, ‘Karen, ulimwengu umezorota.’ Alifadhaishwa hasa na namna ambavyo watoto hutendwa vibaya.
“Hata kabla ya kumtia moyo, akasema kwa ghafula: ‘Wanawake wawili walikuja nyumbani kwangu leo. Kwa kawaida mimi huwa katika bustani yangu nyuma ya nyumba, lakini walinikuta nikiwa upande wa mbele. Mwanamke mmoja alinionyesha picha ya bustani maridadi. Nilitaka kumwambia, “Kwa kweli, wapaswa kuona ua wangu ulio nyuma ya nyumba—ni bustani maridadi,” lakini sikumwambia. Kisha akasema kuwa karibuni kutakuwa na amani ulimwenguni pote. Alisema kwamba utakuwa kama bustani hiyo, itakayompendeza kila mtu. Sikuchukua kitabu hicho. Lakini baada ya wao kuondoka, singeweza kuisahau picha hiyo. Niliendelea tu kuifikiria na kufikiria wazo la amani kwa kila mtu. Je, wajua ni kitabu kipi ninachomaanisha? Je, waweza kuniletea nakala?’”
Karen alifurahi kufanya hivyo. Picha ambayo baba yake alikuwa akirejezea ni ile iliyopo hapa. Kitabu hicho chaitwa Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Je, ungependa kujua mengi juu ya ahadi ya Biblia ya kwamba karibuni Mungu ataifanya dunia iwe bustani ya tufeni pote ambamo watu wataishi kwa amani? Unaweza kupokea nakala ya kitabu hicho kwa kujaza na kupeleka kuponi iliyopo hapa kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ihusuyo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni nakala ya kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia la nyumbani bila malipo.