‘Walikuwa Wazuri Kweli Kweli!’
HIVI karibuni, meneja mkuu wa hoteli moja iliyo karibu na mojawapo ya viwanja vya ndege vya kimataifa nchini Japani alizuru ofisi ya tawi ya Mashahidi wa Yehova katika Ebina. Alisisimuka sana. Kwa nini?
Mnamo mwaka wa 1998, zaidi ya Mashahidi 200 walikaa kwenye hoteli ya meneja huyo walipokuwa wakielekea na kurudi kutoka kwenye mikusanyiko yao ya kimataifa katika Afrika, Australia, Korea, na Amerika Kaskazini. Wakati wafanyakazi wa hoteli hiyo walipokuwa na mkutano wa kupitia utendaji wa mwaka uliotangulia, walisema kwamba kati ya wageni 30,000 ambao huzuru hoteli hiyo kila mwaka, wajumbe hao wa mkusanyiko ndio watu wenye kupendeza zaidi waliopata kuwatumikia.
Kwa hiyo, meneja wa hoteli hiyo alisafiri hadi Ebina ili kuonyesha shukrani zake. ‘Wageni hao,’ akasema, ‘walikuwa wapole sana na waliacha vyumba vyao vikiwa safi na nadhifu. Mara nyingi walionyesha shukrani zao. Isitoshe, walitueleza mambo yenye kutia moyo kutoka kwenye Biblia. Walikuwa wazuri kweli kweli!’
Meneja huyo aliendelea kusema hivi: ‘Sisi huona wageni wengi ambao wamefadhaika. Kwa hiyo tumekuwa tukitafuta habari inayoweza kuwasaidia. Tungependa wajinufaishe na fundisho la Biblia kwa sababu hilo hutokeza badiliko zuri katika maisha ya watu.’
Tokeo lilikuwa kwamba meneja huyo aliagiza nakala 80 za vichapo kadhaa vya Mashahidi wa Yehova ili aviweke kwenye vyumba vya hoteli. Kitabu chenye kurasa 192 Siri ya Kupata Furaha ya Familia kilikuwa miongoni mwa vichapo vilivyoagizwa. Ikiwa ungependa nakala, tafadhali jaza kuponi iliyopo hapa na kuipeleka kwa anwani iliyoonyeshwa au kwa anwani ifaayo iliyoorodhesha kwenye ukurasa wa 5 wa gazeti hili.
□ Nipelekeeni kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia.
□ Tafadhali wasilianeni nami kuhusu funzo la Biblia nyumbani bila