Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g01 12/8 uku. 21
  • Jina la Mungu Lazusha Ubishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jina la Mungu Lazusha Ubishi
  • Amkeni!—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Jina la Mungu na Watafsiri wa Biblia
    Jina la Mungu Litakaloendelea Milele
  • A4 Jina la Mungu Katika Maandiko ya Kiebrania
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Jina la Mungu—Maana na Matumizi
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Je, Ni Kosa Kutamka Jina la Mungu?
    Amkeni!—1999
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2001
g01 12/8 uku. 21

Jina la Mungu Lazusha Ubishi

NA MWANDISHI WA AMKENI! NCHINI UHOLANZI

KAZI ya watafsiri wa Biblia moja ya Kiholanzi imechambuliwa vikali na wasomi wa Biblia na watu wa kawaida. Kwa nini? Ni kwa sababu watafsiri hao waliamua kutafsiri jina la Mungu kuwa Heer, au Bwana.

Mnamo Desemba 1998, majuma machache tu baada ya watafsiri hao kuchapisha sehemu ya Biblia hiyo, kikundi kimoja cha wanawake wa shirika la Protestanti la Kerk en Wereld (Kanisa na Ulimwengu), kilianzisha kampeni ya kupinga neno hilo kwa kuandika barua. Kwa nini? Wanawake hao waliliona neno “Bwana” kuwa linawakilisha “mwanamume.” Punde si punde, vikundi vingine—vya Katoliki na Protestanti—vikaunga mkono kampeni hiyo. Mnamo Februari 1999, wasomi watatu walisema kwamba walipendelea zile herufi nne za Kiebrania za jina la Mungu, YHWH, zisitafsiriwe. Punde baadaye, wasomi wa Biblia, watafsiri, na wanatheolojia, walikutana huko Amsterdam ili kulijadili suala hilo. Baada ya mazungumzo hayo, washiriki wote waliombwa wapige kura ili kuchagua tafsiri waliyopendelea.

Gazeti la Nieuwsblad van het Noorden liliripoti matokeo ya kura hiyo chini ya kichwa ‘Ikiwa Twamheshimu Mungu, Tusipigane Juu ya Jina Lake’ kwa kusema hivi: “Neno BWANA limepigiwa kura saba tu. Tafsiri nyingine pia hazijapigiwa kura nyingi: Jina (1), Aliye (3), Mwenye Rehema (6), Asiyeweza Kupewa Jina (7), Aliye Hai (10), na Aliye wa Milele (15). Tafsiri iliyopigiwa kura nyingi zaidi ni . . . YHWH!” Mnamo Machi 15, 2001, Kamati ya Usimamizi wa tafsiri hiyo mpya ya Biblia iliamua kutumia jina HEER (BWANA) katika herufi kubwa za saizi ndogo kuwakilisha jina la Mungu.

Ubishi huo unaonyesha kwamba japo kuna kutoelewana kuhusu tafsiri bora ya jina la Mungu katika Kiholanzi, wasomi wanakubali kwamba Mungu ana jina. Katika Kiebrania, jina hilo linaandikwa kwa herufi nne za Kiebrania, yaani, יהוה, au YHWH. Biblia nyingine za Kiholanzi, iwe ni za zamani au za sasa, zimetafsiri YHWH jinsi gani?

Mholanzi mmoja aliyeitwa Nicolaas Goetzee alichapisha Biblia ya Staten yenye kurasa zinazoelekeana katika mwaka wa 1762. Kwenye ukurasa wenye kichwa, Biblia hiyo ilisema hivi: “Kwa sababu za maana sana na zinazojulikana sana, hatukutafsiri pia Jina la Ukumbusho la Mungu YEHOVA.” Wasomi wengine Waholanzi walio maarufu—kama Profesa Nicolaas Beets na Petrus Augustus de Genestet—wametumia pia jina Yehova.

Kwa kupendeza, New World Translation of the Holy Scripturesa hutumia jina Yehova kila mahala ambapo jina hilo lapasa kutumiwa. Nyongeza ya Biblia ya New World Translation ya Kiholanzi husema kwamba tafsiri hiyo “huendelea kutumia jina ‘Yehova’ kwa sababu watu wamelizoea kwa karne nyingi. Isitoshe, imetumia . . . zile herufi nne za jina la Mungu, YHWH.” Hivyo, Biblia ya New World Translation imesaidia mamilioni ya watu wajue kweli kuhusu jina la Mungu.

[Maelezo ya Chini]

a Iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki