Usiku wa Kukumbukwa
Kutana Pamoja Nasi—Alhamisi, Aprili 9, 2009
Usiku uliotangulia kifo chake, Yesu Kristo alianzisha Ukumbusho wa kifo chake, akitumia divai na mkate usiotiwa chachu kama mifano. Yesu aliamuru hivi: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”—Luka 22:19.
Mashahidi wa Yehova wanakualika kwa uchangamfu ujiunge nao kutii maneno hayo ya Yesu kwa kukumbuka tukio hilo la kila mwaka. Ili kufahamu mahali pa kukutania, siku na saa, tafadhali wasiliana na Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe.