Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g22 Na. 1 kur. 10-12
  • 3 | Linda Mahusiano Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 3 | Linda Mahusiano Yako
  • Amkeni!—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA NINI NI MUHIMU?
  • Unachopaswa Kujua
  • Unachoweza Kufanya Sasa
  • Marafiki Wazuri na Wabaya
    Amkeni!—2004
  • Chagua Marafiki Wako kwa Hekima
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kutosheleza Tamaa Yetu ya Kuwa na Marafiki
    Amkeni!—2004
  • Kudumisha Urafiki Katika Ulimwengu Usio na Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2022
g22 Na. 1 kur. 10-12
Wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa wakikumbatiana kwa furaha.

ULIMWENGU WENYE MISUKOSUKO

3 | Linda Mahusiano Yako

KWA NINI NI MUHIMU?

Watu wengi wameruhusu bila kutambua mahusiano yao yaharibike, kwa sababu ya mahangaiko yanayosababishwa na hali za ulimwengu zinazozidi kuwa mbaya.

  • Watu wamejitenga na marafiki zao.

  • Wenzi wa ndoa hawatendeani kwa fadhili.

  • Wazazi hawajali mahangaiko ya watoto wao.

Unachopaswa Kujua

  • Ni muhimu kuwa na marafiki kwa sababu watakusaidia kuwa na afya njema ya kimwili na kihisia hasa unapokabili hali ngumu.

  • Mkazo unaoletwa na hali mbaya za ulimwengu, unaweza kusababisha matatizo katika familia yako katika njia zisizotarajiwa.

  • Taarifa za habari zinazoshtua, zinaweza kuwaathiri watoto wako kwa kiasi kikubwa kuliko unavyoweza kutarajia.

Unachoweza Kufanya Sasa

Biblia inasema hivi: “Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”​—Methali 17:17.

Mfikirie mtu ambaye anaweza kukusaidia na kukupa ushauri unaofaa. Kuwa na marafiki wanaokujali, kutakusaidia kupata nguvu za kuvumilia changamoto za kila siku.

JINSI YA KUKABILIANA NA HALI​—Madokezo Yanayofaa

Wakati wa misukosuko, linda mahusiano yako kwa kuchukua hatua hizi zinazofaa

IMARISHA NDOA YAKO

Wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa wakikumbatiana kwa furaha.

Imarisha ndoa yako

Biblia inasema hivi: “Wawili ni afadhali kuliko mmoja . . . Kwa maana mmoja wao akianguka, mwenzake anaweza kumwinua.” (Mhubiri 4:9, 10) Wenzi wa ndoa wanapaswa kutenda kama rubani na msaidizi wake walio na ratiba moja ya safari badala ya kuwa kama marubani wa ndege mbili za kivita zinazopambana.

  • Azimia kutogombana na mwenzi wako kwa sababu ya mikazo mnayokabili. Uwe mwenye subira na uvumilivu.

  • Angalau mara moja kila juma, zungumza na mwenzi wako kuhusu matatizo yoyote mliyonayo. Kumbukeni kushughulikia tatizo, badala ya kugombana.

  • Tumieni wakati pamoja kwa kufanya mambo mnayofurahia.

  • Kumbukeni pindi nzuri mlizofurahia pamoja, kwa mfano, kwa kutazama picha za siku yenu ya harusi, au mambo mengine mazuri.

“Huenda wenzi wa ndoa wasikubaliane katika kila jambo, lakini hilo halimaanishi kwamba hawawezi kushirikiana. Wenzi wa ndoa wanaweza kufanya uamuzi pamoja, na kujitahidi kuutekeleza.”​—David.

DUMISHA URAFIKI WAKO

  • Wanawake kutoka jamii mbalimbali wakicheka na kufurahia kuwa pamoja.

    Dumisha urafiki wako

    Mbali na kupokea msaada kutoka kwa marafiki zako, fikiria pia jinsi unavyoweza kuwasaidia. Unapowaimarisha wengine, utaimarishwa pia.

  • Wajulie hali baadhi ya rafiki zako kila siku.

  • Waulize rafiki zako jinsi walivyokabiliana na changamoto unazopitia.

“Unahitaji marafiki unapokabili matatizo. Wanaweza kukusaidia kujua jambo unalopaswa kufanya. Hata kama watafanya hivyo kwa kukueleza mambo ambayo tayari unajua. Marafiki wanaokujali wanajua kwamba wewe pia unawajali.”​—Nicole.

KUWA KARIBU NA WATOTO WAKO

Wazazi na watoto wao wawili wakiwa wamekaa katika gati wakifurahia mandhari inayowazunguka.

Kuwa karibu na watoto wako

Biblia inasema hivi: “[Uwe] mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema.” (Yakobo 1:19) Huenda mwanzoni watoto wako wakasita kukuambia kuhusu mambo wanayoogopa na yanayowahangaisha, lakini kwa kuwasikiliza kwa subira utawasaidia wajieleze.

  • Fanya iwe rahisi kwa watoto wako kujieleza. Baadhi ya watoto hujihisi huru kujieleza wanapokuwa wamestarehe, kama vile mnaposafiri kwenye gari au mnapotembea, badala ya kuzungumza nao uso kwa uso.

  • Hakikisha kwamba watoto wako hawatazami habari nyingi zenye kushtua.

  • Waeleze watoto wako hatua unazochukua ili kuilinda familia yako.

  • Weka mpango kuhusu mambo ya kufanya wakati wa dharura, na uwazoeze watoto wako.

“Zungumza na watoto wako na uwaruhusu waeleze jinsi wanavyohisi. Huenda wanaficha mambo wanayoogopa, yanayowahangaisha, au yanayowakasirisha. Pia, waambie kwamba unakabili hisia kama hizo, na uwaeleze jinsi unavyozishughulikia.”​—Bethany.

Sehemu ya video yenye kichwa, “Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha.” Wenzi wa ndoa wenye furaha wakiwa wanatembea huku wameshikana mikono.

JIFUNZE MENGI ZAIDI. Tazama video yenye kichwa, Unaweza Kuwa na Familia Yenye Furaha.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki