Sura ya 19
Kupenda Ndugu na Dada Zetu
UNA ndugu na dada wangapi?— Si kila mtu ana ndugu au dada katika jamaa yake nyumbani. lkiwa una hata mmoja, unaweza kushukuru.
Mungu alitufanya tujione kuwa karibu sana na watu fulani. Huenda tukawa na rafiki wengi, lakini ndugu na dada wanatunzana kwa kawaida hata zaidi kuliko na rafiki. Wakati tunakuwa katika taabu, mwingine anasaidia. Ndiyo namna ya ndugu ambaye ungetaka uwe naye, sivyo?—
Lakini si kila mtu ni mzuri kwa ndugu au dada yake. Biblia inatuambia juu ya mtu aliyempiga ndugu yake. Je unajua jina lake?— Alikuwa Kaini, mtoto wa mtu wa kwanza.
Siku moja Kaini alichukua chakula fulani alichokuwa amelima kama mkulima. Akatoa zawadi au toleo la chakula hiki kwa Yehova. Ndugu yake Habili vile vile alitoa toleo kwa Yehova. Habili alitoa kwa Mungu kondoo aliye bora sana ambaye alikuwa naye. Mungu alipendezwa na Habili na toleo lake. Lakini hakupendezwa na Kaini na toleo lake.
Sababu gani ilikuwa hivyo?— Haikuwa kwa sababu Habili alitoa kilicho bora. Na haikuwa toleo lake Ia kondoo lililofanya tofauti. Biblia inatuambia kwamba Mungu aweza kuona yali-yomo katika mioyo ya watu. Yeye anajua namna tunavyoona ndani ndani yetu wenyewe.
Mungu aliona nini katika moyo wa Kaini?— Aliona kwamba Kaini hakumpenda kweli ndugu yake. Kaini aliweza kuona kwamba Yehova alipendezwa na Habili na toleo lake. Lakini je! Kaini alijaribu kugeuka awe kama ndugu yake?— Hapana. Alikasirika.
Yehova alimwambia Kaini kwamba imempasa ageuze njia zake. Lakini Kaini hakusikiliza. lkiwa kweli alikuwa amempenda Mungu, angalimsikiliza. Lakini yeye hakumpenda Mungu. Naye hakumpenda ndugu yake.
Basi, siku moja alimwambia Habili: “Twende uwandani.” Kaini alikuwa na ubaya katika moyo wake, lakini Habili hakujua. Habili akaenda na Kaini. Walipokuwa uwandani peke yao, Kaini akampiga nduguye. Alimpiga kwa nguvu sana hata akamwua. Je! hilo halikuwa jambo baya?— Mwanzo 4:2-8.
Biblia inatuambia kwamba kuna sababu ya pekee kwamba imetupasa tujifunze hilo. Unajua ni nini?— “Hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi, si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu.” Basi ndugu na dada imewapasa wapendane wao kwa wao. Wasiwe kama Kaini.—1 Yohana 3:11, 12.
Sababu gani ingekuwa vibaya sana kuwa kama Kaini?— Kwa sababu Biblia yasema “alivyokuwa wa yule mwovu.” Kwa kuwa Kaini alitenda kama Ibilisi, ilikuwa kana kwamba Ibilisi alikuwa baba yake. Fikiria hilo!
Unafahamu sababu gani ni jambo la maana sana kuwapenda ndugu na dada zako?— Usipowapenda, utakuwa mtoto wa nani?— Ungekuwa mtoto wa Ibilisi. Usingetaka uwe mtoto wa Ibilisi. Usingetaka uwe hivyo, sivyo?— Basi unawezaje kuonyesha unataka kuwa mtoto wa Mungu?— Ni kwa kuwapenda ndugu na dada zako kweli.
Lakini upendo ni nini?— Upendo ni maono mengi ya ndani katika sisi yatufanyayo kutaka kufanya mazuri kwa watu wengine. Tunaonyesha twawapenda wengine tunapokuwa na maono mazuri kwao. Tunaonyesha wakati tunapowafanyia mazuri. Na ikiwa twampenda mtu fulani kweli kweli, je! tutangojea mpaka yeye kwanza atufanyie mazuri ndipo sisi tumfanyie mazuri?—
Mungu hafanyi hivyo. Hata sisi tulipokuwa hatujampenda Mungu, Mungu alitupenda sisi. Twaweza kujifunza kwa hili. Hata wakati wengine hawajatuonyesha sisi upendo, twaweza kuonyesha kwamba twawapenda.
Biblia inasema Wakristo wanao ndugu na dada wengi zaidi kuliko wale ambao wanaishi nyumba moja nao. Unawajua ni akina nani? — Yesu alisema: ‘Ye yote afanyaye mapenzi ya Baba yangu mbinguni ndiye ndugu na dada yangu.’ Maana yake wote wafanyao mapenzi ya Mungu ndio ndugu na dada. Wao ni jamaa ya pekee ya ndugu na dada. Ulijua hilo?— Mathayo 12:50.
Je! unawapenda ndugu na dada wote katika jamaa kubwa hii ya Kikristo?— Yesu alisema imetupasa. Alisema: ‘Kila mtu atajua ninyi ni wanafunzi wangu ikiwa mnapendana ninyi kwa ninyi.’ Hatuwezi kupenda wachache tu kati yao. Yatupasa tupende ndugu na dada zetu wote.—Yohana 13:35.
Twawezaje kuonyesha kweli twawapenda?— Basi, ikiwa twawapenda, hatutakuwa mbali nao kwa sababu hatutaki kusema nao. Tutakuwa wenye urafiki kwao wote. Sikuzote tutawafanyia mazuri. Na wakati wo wote wakiwa katika taabu, tutawasaidia, kwa sababu kweli sisi ni jamaa kubwa.
Wakati tunapowapenda ndugu na dada zetu wote kweli kweli, inaonyesha nini?— Inaonyesha sisi ni wanafunzi wa Yesu, Mwalimu Mkuu. Na sivyo tunavyotaka tuwe?—
(Kuonyesha upendo kwa ndugu na dada zetu tena kunazungumzwa katika 1 Yohana 4:8, 20, 21 na Wagalatia 6:10. sababu gani usifungue Biblia yako mwenyewe usome maandiko hayo?)