Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 37
  • Hema ya Ibada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hema ya Ibada
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Maskani ya Ibada
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kutoka—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • Mwaliko wa Pekee wa Yehova wa Kuwa Wageni Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 37
Maskani au hema la mkutano lililotumiwa na Waisraeli

HADITHI YA 37

Hema ya Ibada

UNAJUA jengo hili? Ni hema ya pekee ya kuabudia Yehova. Watu walimaliza kuijenga mwaka mmoja baada ya kuondoka Misri. Unajua aliyetoa wazo la kuijenga?

Ni Yehova. Musa alipokuwa katika Mlima Sinai, Yehova alimwambia namna ya kuijenga. Alimwambia ijengwe ili iwe vyepesi kubomolewa. Kwa njia hiyo sehemu zake zingeweza kuchukuliwa mahali pengine, na kuunganishwa tena. Basi Waisraeli walipokuwa wakihama hapa na pale jangwani, walichukua hema hiyo.

Ukitazama ndani ya chumba kidogo mwishoni mwa hema, unaweza kuona sanduku, au kasha. Hilo laitwa sanduku la agano. Kila upande ulikuwa na malaika au kerubi mmoja wa dhahabu. Tena Mungu aliziandika Amri Kumi juu ya mabamba mawili ya mawe, kwa sababu Musa alikuwa ameyavunja yale ya kwanza. Na mawe hayo yalitunzwa ndani ya sanduku la agano. Pia, mtungi wa mana ulitunzwa ndani yake. Unakumbuka mana ni nini?

Yehova anachagua Haruni ndugu yake Musa awe kuhani mkuu. Anawaongoza watu wamwabudu Yehova. Na wanawe ni makuhani pia.

Sasa kitazame chumba kikubwa zaidi cha hema hiyo. Ni kikubwa mara mbili kuliko kile chumba kidogo. Unaliona lile sanduku au kasha dogo, na moshi kidogo ukipanda kutoka ndani yake? Ndiyo madhabahu ambapo makuhani wanachoma uvumba. Halafu kuna kinara cha taa chenye taa saba. Na kitu cha tatu chumbani ni meza. Mikate 12 inatunzwa juu yake.

Bakuli la maji na madhabahu

Uani mwa hema mna bakuli kubwa, au birika, iliyojaa maji. Makuhani wanaitumia kwa kuogea. Pia kuna madhabahu kubwa. Hapo ndipo wanyama wafu wanapochomwa wawe toleo kwa Yehova. Hema iko katikati ya kambi, na Waisraeli wanakaa katika hema zao kuizunguka.

Kutoka 25:8-40; 26:1-37; 27:1-8; 28:1; 30:1-10, 17-21; 34:1, 2; Waebrania 9:1-5.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki