Twataka Kusaidia
Broshua hii imetayarishwa ili ufahamishwe vizuri zaidi utendaji wa Mashahidi wa Yehova na mipango yao ya kukusaidia uongeze maarifa ya Biblia. Labda umepata kutembelewa na Mashahidi wa Yehova safari fulani fulani, au labda umesema nao barabarani au mahali penginepo. Huenda sasa mmoja wa Mashahidi anajifunza pamoja na wewe.
Je! ulijua kwamba ujumbe wao juu ya Ufalme wa Mungu unatangazwa ulimwenguni pote? Kwa sababu gani? Ni kwa sababu Mungu, Muumba wetu, ataka watu kutoka mataifa yote waungane katika kumwabudu yeye. Alitabiri kwa ajili ya wakati wetu hivi: “Mataifa mengi bila shaka yataenda na kusema: ‘Njoni, enyi watu, na tuende juu kwenye mlima wa Yehova, na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo; naye atatuagiza juu ya njia zake, na sisi tutatembea katika vijia vyake.’” —Isaya 2:2, 3, NW.
Utendaji wa Mashahidi wa Yehova katika kukuambia wewe juu ya njia za Mungu ni utimizo wa unabii huo. Kurasa zinazofuata zitaonyesha ni kwa sababu gani utendaji huo ni wa maana sasa na jinsi wewe unavyoweza kufaidika nao.