Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • dg seh. ya 8 kur. 17-19
  • Kusudi la Mungu Lasonga Kuelekea Utimizo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusudi la Mungu Lasonga Kuelekea Utimizo
  • Je, Kweli Mungu Anatujali?
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mfalme Mpya wa Dunia
  • Watawala Washirika
  • Utawala wa Kujitegemea Kukoma
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufalme wa Mungu—Utawala Mpya wa Dunia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Ufalme wa Mungu Watawala
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
Pata Habari Zaidi
Je, Kweli Mungu Anatujali?
dg seh. ya 8 kur. 17-19

Sehemu ya 8

Kusudi la Mungu Lasonga Kuelekea Utimizo

1, 2. Mungu amekuwa akifanyaje uandalizi kuondolea mbali kuteseka?

UTAWALA wa wanadamu waasi na wa roho waovu umekuwa ukikokota familia ya kibinadamu kuelekea chini kwa karne nyingi. Hata hivyo, Mungu hakupuuza kuteseka kwetu. Badala ya hivyo, wakati wa karne zote, yeye amekuwa akifanya uandalizi ili kufungua wanadamu katika uovu na kuteseka.

2 Wakati wa uasi ule katika Edeni, Mungu alianza kufunua kusudi lake la kuunda serikali ambayo ingefanya dunia hii kuwa makao ya paradiso kwa ajili ya watu. (Mwanzo 3:15) Baadaye, akiwa mneni mkuu wa Mungu, Yesu alifanya serikali hiyo ya Mungu iliyokuwa ikija kuwa kichwa cha mafundisho yake. Yeye alisema kwamba hiyo ingekuwa tumaini pekee la ainabinadamu.—Danieli 2:44; Mathayo 6:9, 10; 12:21.

3. Yesu aliiitaje serikali iliyokuwa ikija kwa ajili ya dunia, na kwa nini?

3 Yesu aliiita serikali hiyo ya Mungu iliyokuwa ikija “ufalme wa mbinguni,” kwa kuwa ingetawala kutoka mbinguni. (Mathayo 4:17) Aliiita pia “ufalme wa Mungu,” kwa kuwa Mungu angekuwa Mwanzilishi wayo. (Luka 17:20) Kwa karne zilizopita Mungu aliongoza kwa roho waandikaji wake waandike unabii mwingi juu ya wale ambao wangejumuika kuwa serikali hiyo na mambo ambayo ingetimiza.

Mfalme Mpya wa Dunia

4, 5. Mungu alionyeshaje kwamba Yesu alikuwa Mfalme aliyekubaliwa naye?

4 Yesu ndiye, karibu miaka elfu mbili iliyopita, aliyetimiza unabii mwingi juu ya yule ambaye angekuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu. Alithibitika kuwa chaguo la Mungu la Mtawala wa serikali hiyo ya kimbingu juu ya ainabinadamu. Baada ya kifo chake, Mungu alimfufua Yesu kwenda kwenye uhai katika mbingu akiwa kiumbe-roho mwenye nguvu, asiyeweza kufa. Walikuwako mashahidi wengi wa kufufuliwa kwake.—Matendo 4:10; 9:1-9; Warumi 1:1-4; 1 Wakorintho 15:3-8.

5 Ndipo Yesu ‘alipoketi mkono wa kuume wa Mungu.’ (Waebrania 10:12) Hapo alingoja wakati wa Mungu wa kumpa mamlaka achukue hatua akiwa Mfalme wa Ufalme wa kimbingu wa Mungu. Hilo lilitimiza unabii kwenye Zaburi 110:1, ambapo Mungu humwambia: “Uketi mkono wangu wa kuume, hata niwafanyapo adui zako kuwa chini ya miguu yako.”

6. Yesu alionyeshaje kwamba alistahili kuwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu?

6 Alipokuwa duniani, Yesu alionyesha kwamba alistahili cheo hicho. Ujapokuwa mnyanyaso, yeye alichagua kudumisha uaminifu-maadili wake kwa Mungu. Kwa kufanya hivyo, yeye alionyesha kwamba Shetani alikuwa mwongo alipodai kwamba hakuna binadamu ambaye angeweza kuwa mwaminifu kwa Mungu chini ya jaribu. Yesu, mwanadamu mkamilifu, yule ‘Adamu wa pili,’ alionyesha kwamba Mungu hakuwa amekosea katika kuwaumba wanadamu wakamilifu.—1 Wakorintho 15:22, 45; Mathayo 4:1-11.

7, 8. Ni mambo gani mema ambayo Yesu alifanya alipokuwa duniani, naye alionyesha nini?

7 Ni mtawala yupi aliyepata wakati wowote kutimiza mema mengi kama alivyofanya Yesu katika miaka michache ya huduma yake? Akitiwa nguvu na roho takatifu ya Mungu, Yesu aliponya wagonjwa, vilema, vipofu, viziwi, na wasionena. Hata alifufua wafu! Alionyesha kwa kadiri ndogo mambo ambayo angefanyia ainabinadamu kwa kadiri ya tufe lote wakati yeye angekuja katika mamlaka ya Ufalme.—Mathayo 15:30, 31; Luka 7:11-16.

8 Yesu alifanya mema mengi sana alipokuwa duniani hivi kwamba mwanafunzi wake Yohana alisema hivi: “Kuna na mambo mengine mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.”—Yohana 21:25a

9. Kwa nini watu wenye mioyo minyofu walimwendea Yesu makundi makundi?

9 Yesu alikuwa mwenye fadhili na mwenye huruma, akiwa na upendo mwingi kwa watu. Alisaidia maskini na walioonewa, lakini hakubagua wale wenye utajiri au cheo. Watu wenye mioyo minyofu waliitikia ule mwaliko wenye upendo wa Yesu aliposema: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.” (Mathayo 11:28-30) Watu wenye kumhofu Mungu walimwendea makundi makundi na wakatazamia utawala wake.—Yohana 12:19.

Watawala Washirika

10, 11. Ni nani watashiriki pamoja na Yesu katika kutawala juu ya dunia?

10 Kama vile serikali za kibinadamu zilivyo na watawala washirika, ndivyo ulivyo Ufalme wa kimbingu wa Mungu. Wengine zaidi ya Yesu watashiriki katika kutawala juu ya dunia, maana Yesu aliahidi washirika wake wa karibu kwamba wangetawala juu ya ainabinadamu pamoja naye wakiwa wafalme.—Yohana 14:2, 3; Ufunuo 5:10; 20:6.

11 Kwa sababu hiyo, wakiwa pamoja na Yesu, idadi yenye kikomo ya wanadamu itafufuliwa pia kwenye uhai wa kimbingu. Wao hujumuika kuwa Ufalme wa Mungu ambao utaletea ainabinadamu baraka za milele. (2 Wakorintho 4:14; Ufunuo 14:1-3) Hivyo muda wa enzi zote, Yehova ameweka msingi kwa ajili ya utawala ambao utaletea familia ya kibinadamu baraka za milele.

Utawala wa Kujitegemea Kukoma

12, 13. Ufalme wa Mungu sasa uko tayari kufanya nini?

12 Katika karne hii Mungu amehusika moja kwa moja katika mambo ya dunia. Kama vile Sehemu ya 9 ya broshua hii itakavyozungumza, unabii wa Biblia huonyesha kwamba Ufalme wa Mungu chini ya Kristo ulisimamishwa katika 1914 na sasa uko tayari kuponda-ponda mfumo wote wa Shetani. Ufalme huo uko tayari ‘kwenda ukitiisha kati ya adui za [Kristo].’—Zaburi 110:2, NW.

13 Kwa habari hii unabii kwenye Danieli 2:44 husema hivi: “Na katika siku za wafalme hao [waliopo sasa] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme [mbinguni] ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake [utawala wa kibinadamu hautaruhusiwa tena kamwe]; bali [Ufalme wa Mungu] utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”

14. Ni baadhi ya faida zipi zitakazokuja kama tokeo la kukoma kwa utawala wa kibinadamu?

14 Utawala wote wa kujitegemea bila Mungu ukiwa umeondolewa mbali, utawala wa Ufalme wa Mungu juu ya dunia utakuwa kamili. Na kwa sababu Ufalme hutawala kutoka mbinguni, hauwezi kufisidiwa kamwe na wanadamu. Mamlaka ya kutawala itakuwa mahali ilipokuwa mwanzoni, yaani, mbinguni, ikiwa na Mungu. Na kwa kuwa utawala wa Mungu utakuwa ukidhibiti dunia yote, hakuna mtu atakayeongozwa vibaya tena na dini bandia au falsafa za kibinadamu na nadharia za kisiasa zisizoridhisha. Hakuna lolote la mambo hayo litakaloruhusiwa kuwako.—Mathayo 7:15-23; Ufunuo sura za 17 hadi 19.

[Maelezo ya Chini]

a Ili kupata habari kamili juu ya maisha ya Yesu, ona kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, kilichotangazwa 1991 na Watchtower Society.

[Picha katika ukurasa wa 18]

Alipokuwa duniani Yesu aliponya wagonjwa na kufufua wafu ili kuonyesha mambo ambayo angefanya katika ulimwengu mpya

[Picha katika ukurasa wa 19]

Ufalme wa kimbingu wa Mungu utaponda- ponda na kuziondolea mbali zisiwepo namna zote za utawala wa kujitegemea bila yeye

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki