Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • gf somo la 15 kur. 24-25
  • Rafiki za Mungu Hufanya Mambo Mema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Rafiki za Mungu Hufanya Mambo Mema
  • Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Funguo Mbili za Kuwa na Ndoa Yenye Kudumu
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Maisha ya Familia Yanayompendeza Mungu
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Kwa Nini Unapaswa Kuheshimu Mamlaka?
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo la 15 kur. 24-25

SOMO LA 15

Rafiki za Mungu Hufanya Mambo Mema

Ukiwa na rafiki unayempenda na kumheshimu, wewe hujaribu kuwa kama yeye. “BWANA yu mwema, mwenye adili,” Biblia yasema. (Zaburi 25:8) Ili tuwe rafiki za Mungu, ni lazima tuwe watu wema na wenye adili. Biblia inasema hivi: “Iweni waigaji wa Mungu, mkiwa watoto wapendwa, na endeleeni kutembea katika upendo.” (Waefeso 5:1, 2) Hapa pana njia kadhaa za kufanya hivyo:

Wasaidie wengine. “Acheni sisi tufanye lililo jema kuelekea wote.”—Wagalatia 6:10.

Fanya kazi kwa bidii. “Mwibaji na asiibe tena, bali acheni afanye kazi ya bidii, akifanya kwa mikono yake kazi iliyo njema.”—Waefeso 4:28.

Dumu ukiwa safi kimwili na kiadili. “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na wa roho, tukikamilisha utakatifu katika hofu ya Mungu.”—2 Wakorintho 7:1.

Watendee washiriki wa familia yako kwa upendo na heshima. “Acheni kila mtu . . . kati yenu ampende hivyo mke wake kama yeye mwenyewe; kwa upande mwingine, mke apaswa kuwa na staha yenye kina kirefu kwa mume wake. Watoto, iweni watiifu kwa wazazi wenu.”—Waefeso 5:33–6:1.

Wapende wengine. “Acheni tuendelee kupendana, kwa sababu upendo ni wa kutoka kwa Mungu.”—1 Yohana 4:7.

Tii sheria za nchi. “Acheni kila nafsi iwe katika ujitiisho kwa [serikali] . . . Walipeni wote haki zao, kwa yeye atakaye kodi, kodi.”—Waroma 13:1, 7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki