Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 1
  • Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina gani?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Thamani za Kiadili Ziletazo Furaha
    Amkeni!—1991
  • Maadili Yanayoboresha Maisha
    Amkeni!—2013
  • Umuhimu wa Kuwa na Maadili
    Amkeni!—2019
  • Mashahidi wa Yehova
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 1

SOMO LA 1

Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

Shahidi wa Yehova nchini Denmark

Denmark

Mashahidi wa Yehova nchini Taiwan

Taiwan

Mashahidi wa Yehova nchini Venezuela

Venezuela

Mashahidi wa Yehova nchini India

India

Unawajua Mashahidi wa Yehova wangapi? Baadhi yetu ni majirani, wafanyakazi, au hata wanafunzi wenzako. Huenda tumewahi kuzungumza nawe kuhusu Biblia. Sisi ni akina nani, na kwa nini tunawaeleza watu kuhusu imani yetu hadharani?

Sisi ni watu wa kawaida. Tumetoka katika malezi na jamii tofauti-tofauti. Baadhi yetu walikuwa wafuasi wa dini mbalimbali na hata wengine hawakuamini kuna Mungu. Hata hivyo, kabla ya kuwa Mashahidi, sote tulichunguza kwa makini mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliamini mambo tuliyojifunza, kisha tukaamua sisi wenyewe kumwabudu Yehova Mungu.

Tunafaidika kwa kujifunza Biblia. Kama watu wengine, sisi pia tunakabiliana na matatizo na udhaifu wetu wenyewe. Lakini kwa kujitahidi kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu ya kila siku, tunajionea mabadiliko makubwa maishani. (Zaburi 128:1, 2) Hiyo ndiyo sababu moja inayofanya tuwaeleze wengine kuhusu mambo mazuri ambayo tumejifunza katika Biblia.

Tunaishi kulingana na viwango vya Mungu. Viwango hivyo tunavyojifunza katika Biblia vinatusaidia kuwa na hali njema na kuwaheshimu wengine, kutia ndani kuwa na sifa kama vile unyoofu na fadhili. Viwango hivyo vinatusaidia pia kuwa watu wazuri na wenye manufaa katika jamii. Isitoshe, vinasaidia familia kuwa na umoja na mwenendo mzuri. Kwa sababu tuna uhakika kwamba “Mungu hana ubaguzi,” sisi ni familia kubwa ya ulimwenguni pote ambayo haina ubaguzi wa kijamii wala wa kisiasa. Ingawa sisi ni watu wa kawaida tu, kuna tofauti kati yetu na vikundi vingine.—Matendo 4:13; 10:34, 35.

  • Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wa kawaida tu?

  • Mashahidi wamejifunza viwango gani katika Biblia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki