Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g91 1/8 kur. 8-9
  • Thamani za Kiadili Ziletazo Furaha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Thamani za Kiadili Ziletazo Furaha
  • Amkeni!—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Matokeo
  • Msingi wa Maadili Yaliyo Bora Zaidi
  • Je! Ni Thamani za Kizamani?
  • Thamani Ambazo Zakufurahisha
  • Umuhimu wa Kuwa na Maadili
    Amkeni!—2019
  • Kutegemezwa na Maadili Yanayodumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Maadili Yanayoboresha Maisha
    Amkeni!—2013
  • Thamani Zinazobadilika Wakati Historia Inapopita
    Amkeni!—1991
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1991
g91 1/8 kur. 8-9

Thamani za Kiadili Ziletazo Furaha

MTOTO angefanya nini akiachwa mbele ya meza iliyojazwa chakula kifaacho na peremende? Kama hangeongozwa na mtu, yaelekea angechagua kula akipendacho zaidi—labda peremende—mpaka awe mgonjwa.

Kiadili, binadamu akabiliwa na machaguo. Yeye ataka nini zaidi? Je! ni maisha ya familia yenye furaha na wakati ujao salama au ni kuishi siku kwa siku kwa kutegemea raha, bila kujali matokeo? Lolote achagualo, chaguo lake litafanyiza maisha yake na kuathiri wakati ujao wake—kwa wema au kwa ubaya.

Matokeo

Tunda la mabadiliko makubwa ya kingono na uhuru usio na vizuizi halijawa jema. Watu waliotenda kama walivyotaka wamekutana na chungu nzima ya matatizo yasiyotakikana: nyumba zilizovunjika, mimba zisizotakikana, kifo kutokana na UKIMWI na magonjwa mengine yenye kuambukizwa kingono, maisha zenye kuharibiwa na utumizi mbaya wa dawa za kulevya, na matokeo mengine yasiyotamaniwa. Matokeo haya mabaya hufaana na elezo lililoandikwa katika Biblia kwenye Mithali 16:25: “Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; lakini mwisho wake ni njia za mauti.”—Ona pia Wagalatia 5:19-21.

Ubinafsi na uhuru ulioenea sana wa kufanya lolote tu bila kujali madaraka walingana na elezo juu ya wakati wetu lipatikanalo kwenye 2 Timotheo 3:1-4, NW: “Katika siku za mwisho nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa. Kwa maana watu watakuwa wajipenda wenyewe, wapenda fedha, wenye kimbelembele, wenye kujigamba, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio waaminifu-washikamanifu, wasio na shauku ya asili, wasiotaka mwafaka wowote, wachongezi, bila kujidhibiti, wakali, bila upendo wa wema, wasaliti, wenye kichwa kigumu, wenye kuvimbishwa kwa kiburi, wapenda raha kuliko kuwa wapenda Mungu.”

Msingi wa Maadili Yaliyo Bora Zaidi

Yote haya yaonyesha uhitaji wa chanzo cha thamani zilizo bora kuliko za binadamu ili tuweze kutembea kwa hekima katika hizi nyakati za hatari. Yeremia, mmoja wa waandikaji wa Biblia, alikiri jambo hili aliposema hivi: “Ee BWANA [Yehova, NW], najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.”—Yeremia 10:23.

Lakini nani awezaye kuweka msingi wa thamani za maadili zilizo bora zaidi? Katika kitabu chake Cours de philosophie, profesa Mfaransa Armand Cuvillier aeleza kwamba yeye, kama wanafalsafa walio wengi, amemchukua “mtu binadamu kuwa ndiye thamani iliyo ya msingi.” Hata hivyo, yeye atukumbusha kwamba kanuni zote za kiadili zenye kutegemea binadamu huwa rahisi kuvunjika na kubadilishwa na nyinginezo baadaye.

Mara nyingi mfanyiza mashine ndiye hustahili zaidi kuifanyisha kazi kwa njia bora zaidi. Ni hivyo hivyo kuhusu Mungu na binadamu. Akiwa ndiye Muumba wa binadamu, Yehova ndiye aliye katika hali bora zaidi kumwonyesha thamani apaswazo kuwa nazo, na kwa nini. Katika Biblia, Yehova hujiita Yule ‘atufundishaye ili tupate faida, atuongozaye kwa njia itupasayo kuifuata.’—Isaya 48:17.

Je! Ni Thamani za Kizamani?

Je! thamani za kiadili za Biblia zaweza kutumiwa kwa wakati wetu? Miaka zaidi ya 1,900 iliyopita, mtume Paulo alitoa orodha ya sifa zitakwazo kwa watumishi wa Mungu. Alitaja “upendo, shangwe, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujidhibiti.” Je! sifa hizi zina thamani pungufu leo? Sivyo kamwe! Ingawa hali zimebadilika, bado kanuni hizi za juu ndizo zilizo bora zaidi.—Wagalatia 5:22, 23, NW.

Yale yale yaweza kusemwa juu ya mambo ambayo Biblia hukataza. Mathalani, kwa nini Mungu aliharibu majiji ya Sodoma na Gomora? Mwanafunzi Yuda alieleza kwamba hii ni kwa sababu wakaaji wayo “walijiachilia kwenye ukosefu wa adili katika ngono na upotovu.” Yuda aongezea kwamba uharibifu wao watumika kuwa “onyo la daima.” Kwa kuwa usimulizi huu na mengine yaliyo kama huo ‘yameandikwa kutuagiza sisi,’ ‘kuwa onyo kwetu,’ masomo ya kiadili ambayo yatokana nayo yangali halali.—Yuda 7, Phillips; Warumi 15:4; 1 Wakorintho 10:11, NW.

Thamani Ambazo Zakufurahisha

Kumbuka kwamba Biblia haina kifani. Ikubali, “si kama neno la wanadamu, bali kama neno la Mungu.” (1 Wathesalonike 2:13) Kati ya mamilioni yote ya vitabu vilivyo ulimwenguni, Biblia pekee ndiyo ‘imevuviwa na Mungu, na yaweza kunyoosha mambo.’ (2 Timotheo 3:16, NW) Hiyo pekee ndiyo iwezayo kutupa sisi thamani zilizo bora zaidi na kuonyesha jinsi ziongozavyo kwenye uhai wa milele katika ulimwengu mpya. Kwa uhakika, mwendo wa hekima ni kuichunguza.

Hivyo hasa ndivyo alivyofanya mwanamume mmoja kijana jina lake Joël. Miaka michache iliyopita, yeye alitembea katika barabara za mji wa kwao nyumbani katika Ufaransa pamoja na vijana wengine—wakiwa na silaha. Alijulikana kuwa mwenye kasirani, naye alikuwa mchuuzi wa dawa za kulevya na mtongozeaji. Joël alijifunza juu ya Biblia na tumaini iletalo, na, baada ya muda, akabadilika kabisa, akiondolea mbali mazoea ambayo hulaaniwa vikali na Biblia. Watu kadhaa kati ya rafiki zake wa zamani walisadiki kwamba ameupata ukweli, hivyo basi wao pia wakafanya mabadiliko makubwa katika maisha zao na kubatizwa kuwa Mashahidi wa Yehova.

Bila shaka, walio wengi wa ambao walikuja kuwa Mashahidi wa Yehova hawakuendesha maisha yaliyo mbali sana na kanuni za Biblia kama vile Joël na waandamani wake walivyofanya. Lakini wote ambao huja kuwa Mashahidi huafiki kufikiria upya thamani zinazoongoza maisha zao—hata ikiwa hizo zenyewe hazikuwa mbaya—nao husadiki kwamba wamepata mfumo wa thamani ziwezazo kuwafanya wenye furaha.

Kotekote ulimwenguni, Mashahidi karibu milioni nne hujaribu kuishi kulingana na kanuni hizi kila siku, hata iwe wao huishi katika nchi au aina gani ya jamii ya watu. Pia wao huziweka kwanza masilahi za Ufalme wa Mungu, wakitanguliza thamani za kiroho katika maisha zao. Kwa nini usikubali mwaliko wao kukusaidia kuchunguza manufaa ambazo wewe pia waweza kupata kutokana na thamani hizi? “Amani nyingi” yaahidiwa kwa wote wale wanaofanya chaguo hili.—Zaburi 119:165; Mathayo 6:33.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Watu wahitaji thamani zipitazo falsafa za kibinadamu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki