Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jl somo la 21
  • Betheli Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Betheli Ni Nini?
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Hii Yaweza Kuwa Kazi-Maisha Inayokufaa Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kutazama “Nyumba ya Mungu” kwa Uthamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Je, Waweza Kujitolea?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Watu Wote Wanaalikwa!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
jl somo la 21

SOMO LA 21

Betheli Ni Nini?

Mashahidi wawili wa Yehova wakifanya kazi Betheli katika Idara ya Uchoraji

Idara ya Uchoraji, Marekani

Shahidi wa Yehova akifanya kazi katika kiwanda cha kuchapisha cha Betheli kilicho nchini Ujerumani

Ujerumani

Shahidi wa Yehova akifanya kazi katika dobi ya Betheli iliyo nchini Kenya

Kenya

Wahudumu wakiweka vyakula mezani katika chumba cha kulia chakula cha Betheli nchini Kolombia

Kolombia

Betheli ni neno la Kiebrania linalomaanisha “Nyumba ya Mungu.” (Mwanzo 28:17, 19, maelezo ya chini) Ni jina linalofaa ambalo Mashahidi wa Yehova hutumia kurejelea majengo yaliyoko katika nchi mbalimbali ambapo mwongozo na msaada kuhusiana na kazi ya kuhubiri unatolewa. Baraza Linaloongoza linafanya kazi likiwa katika makao makuu katika Jimbo la New York, Marekani, na kutoka huko linasimamia kazi inayofanywa na ofisi za tawi katika nchi mbalimbali. Wakiwa pamoja, wote wanaofanya kazi katika ofisi hizo wanaitwa familia ya Betheli. Kama familia, wanaishi na kufanya kazi pamoja, na wanakula na kujifunza Biblia pamoja kwa umoja.—Zaburi 133:1.

Mahali pa pekee ambapo washiriki wanajitolea kwa hiari. Katika kila ofisi ya Betheli kuna wanaume na wanawake Wakristo ambao wamejitolea kufanya mapenzi ya Mungu na kuendeleza masilahi ya Ufalme kwa wakati wote. (Mathayo 6:33) Hakuna yeyote kati yao anayepokea mshahara. Wote wanapewa mahali pa kulala, chakula, na pesa kidogo kwa ajili ya matumizi ya kibinafsi. Kila Mwanabetheli ana mgawo wake, huenda ikawa ni ofisini, jikoni, au katika chumba cha kulia chakula. Wengine wanafanya kazi ya kuchapisha vitabu, kutunza vyumba, kufua nguo, kudumisha majengo, au kazi nyingine.

Sehemu yenye shughuli nyingi inayosaidia kazi ya kuhubiri Ufalme. Kusudi kuu la Betheli ni kufanya ujumbe wa kweli wa Biblia uwafikie watu wengi iwezekanavyo. Mfano mmoja ni broshua hii. Iliandikwa chini ya usimamizi wa Baraza Linaloongoza, ikatumwa kwa mamia ya vikundi vya watafsiri ulimwenguni pote, ikachapishwa katika mashine zenye uwezo mkubwa zinazopatikana katika Betheli kadhaa, na hatimaye ikatumwa katika makutaniko zaidi ya 110,000. Katika kila hatua ya kazi hii, familia za Betheli zinatekeleza huduma za lazima ili kutegemeza kazi muhimu kuliko zote, kazi ya kuhubiri habari njema.—Marko 13:10.

  • Ni nani wanaofanya kazi Betheli, na wanatunzwa jinsi gani?

  • Ni kazi gani muhimu inayotegemezwa na huduma zinazotekelezwa Betheli?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki