Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bhs kur. 3-7
  • Mungu Alituumba kwa Kusudi Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Alituumba kwa Kusudi Gani?
  • Biblia Inatufundisha Nini?
  • Soma katika Biblia Inafundisha
  • Vichwa vidogo
  • BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATAFANYA MAMBO MAZURI DUNIANI.
  • FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA
Biblia Inatufundisha Nini?
bhs kur. 3-7

Mungu Alituumba kwa Kusudi Gani?

UNAPOSOMA magazeti, kutazama televisheni, au kusikiliza redio unapata habari nyingi kuhusu uhalifu, vita, na ugaidi. Huenda wewe pia unateseka kwa sababu ya ugonjwa au umefiwa na mpendwa wako.

Familia ikisikiliza habari kwenye redio

Hebu jiulize:

  • Je, Mungu alikusudia maisha yangu na ya familia yangu yawe hivi?

  • Ninaweza kupata wapi msaada wa kukabiliana na matatizo yangu?

  • Je, inawezekana kuwa na amani duniani?

Biblia inajibu maswali hayo kwa njia yenye kuridhisha.

BIBLIA INAFUNDISHA KWAMBA MUNGU ATAFANYA MAMBO MAZURI DUNIANI.

  • Hakutakuwa na maumivu, kuzeeka, au kifo.—Ufunuo 21: 4

  • “Kilema ataruka kama paa.” —Isaya 35:6

  • “Macho ya vipofu yatafunguliwa.”—Isaya 35:5

  • Wafu watafufuliwa.—Yohana 5:28, 29

  • Hakuna atakayekuwa mgonjwa. —Isaya 33:24

  • Dunia itakuwa na chakula tele. —Zaburi 72:16

    Wazee wanakuwa vijana, vilema wanaruka, wafu wanafufuliwa, wagonjwa na vipofu wanaponywa

FAIDIKA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA

Shahidi wa Yehova anajifunza Biblia na mwanamume fulani

Usidhani kwamba mambo uliyosoma kwenye kurasa zilizotangulia ni ndoto tu. Mungu ameahidi kutimiza mambo hayo hivi karibuni, na Biblia inaeleza jinsi atakavyofanya.

Biblia inafundisha mambo mengine mengi zaidi ya hayo. Inatueleza mambo ya kufanya ili tuwe na maisha yenye furaha sasa. Hebu fikiria mambo yanayokufanya uwe na wasiwasi. Labda ni kuhusu pesa, matatizo ya familia, afya, au kifo cha mpendwa wako. Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na matatizo hayo, na inaweza kukufariji kwa kujibu maswali yafuatayo:

  • Kwa nini tunateseka?

  • Tunawezaje kukabiliana na matatizo yetu?

  • Je, inawezekana kuwa na familia yenye furaha?

  • Inakuwaje mtu akifa?

  • Je, tutawaona tena wapendwa wetu waliokufa?

  • Kwa nini tunaweza kuwa na uhakika kwamba Mungu atatimiza mambo yote aliyoahidi??

Kusoma kitabu hiki kunaonyesha kwamba unataka kujua yale ambayo Biblia inafundisha. Kitabu hiki kitakusaidia. Chini ya kurasa kuna maswali ambayo yatakusaidia kuielewa vizuri Biblia. Mamilioni ya watu wamefurahia kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Tunatumaini wewe pia utafurahia. Mungu na akubariki unapojitahidi kujifunza yale ambayo Biblia inafundisha!

IJUE BIBLIA YAKO

BIBLIA ina vitabu 66. Kila kitabu kina sura na mistari ili kurahisisha usomaji. Maandiko yanapotajwa katika kitabu hiki, namba inayofuata jina ni sura ya kitabu katika Biblia, nayo namba inayofuata ni mstari. Kwa mfano, “2 Timotheo 3:16,” ni barua ya pili kwa Timotheo, sura ya 3, mstari wa 16.

Ukifungua na kusoma maandiko yaliyo katika kitabu hiki, utazoea kuitumia Biblia. Pia, weka lengo la kusoma Biblia kila siku. Ukisoma sura tatu hadi tano hivi kila siku, unaweza kusoma Biblia nzima kwa mwaka mmoja.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki