Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 34 uku. 84-uku. 85 fu. 2
  • Gideoni Aliwashinda Wamidiani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Gideoni Aliwashinda Wamidiani
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • “Upanga wa Yehova na wa Gideoni!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Gideoni na Wanaume Wake 300
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Wazee—Jifunzeni Kutokana na Mfano wa Gideoni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • “Kila Mtu Mahali Pake”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 34 uku. 84-uku. 85 fu. 2
Gideoni na askari wake wakipiga pembe, wakivunja mitungi, wakinyoosha mienge, na kupaza sauti

SOMO LA 34

Gideoni Aliwashinda Wamidiani

Baada ya muda, Waisraeli walimwacha tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uwongo. Kwa miaka saba, Wamidiani waliiba mifugo na kuharibu mazao ya Waisraeli. Kwa hiyo, ili kuwatoroka Wamidiani, Waisraeli walijificha kwenye mapango na milima. Wakamwomba Yehova awasaidie. Hivyo, Yehova alimtuma malaika kwa mwanamume aliyeitwa Gideoni. Malaika akamwambia hivi: ‘Yehova amekuchagua wewe kuwa shujaa mwenye nguvu.’ Gideoni akamuuliza: ‘Ninawezaje kuwaokoa Waisraeli? Sina uwezo wowote.’

Ni nini ambacho kingemthibitishia Gideoni kwamba kwa kweli Yehova alikuwa amemchagua? Gideoni alichukua manyoya ya kondoo na kuyaweka chini, kisha, akamwambia hivi Yehova: ‘Kesho asubuhi nikikuta umande kwenye manyoya lakini eneo lingine liwe kavu, nitajua kwamba umenichagua niwaokoe Waisraeli.’ Kesho yake, manyoya yalikuwa yamelowa lakini ardhi ilikuwa kavu! Kisha, Gideoni akaomba kwamba asubuhi inayofuata, Yehova afanye eneo liwe na umande lakini manyoya yawe makavu. Sala hiyo ilipojibiwa, Gideoni akaamini kabisa kwamba Yehova alikuwa amemchagua. Akakusanya askari wake ili kwenda kupigana na Wamidiani.

Yehova akamwambia hivi Gideoni: ‘Nitawapa Waisraeli ushindi. Lakini kwa kuwa una askari wengi, unaweza kufikiri kwamba mmeshinda kwa nguvu zenu wenyewe. Waambie kwamba ikiwa kuna mtu yeyote anayeogopa, arudi nyumbani.’ Kwa hiyo, askari 22,000 wakarudi nyumbani, na askari 10,000 wakabaki. Kisha, Yehova akasema: ‘Bado una askari wengi sana. Wapeleke kwenye kijito na uwaambie wanywe maji. Baki na wale tu watakaokunywa maji huku wakiangalia maadui.’ Ni wanaume 300 tu waliokuwa macho wakati wanakunywa maji. Yehova aliahidi kwamba wanaume hao wachache watalishinda jeshi la Midiani lenye askari 135,000.

Usiku huo, Yehova alimwambia Gideoni hivi: ‘Huu ndio wakati wa kuwashambulia Wamidiani!’ Gideoni aliwapa watu wake pembe na mitungi mikubwa iliyokuwa na mienge ndani yake. Akawaambia hivi: ‘Nitazameni na mfanye kama ninavyofanya.’ Kisha, Gideoni akapiga pembe, akavunja mtungi, akanyoosha mwenge wake, na kusema: ‘Upanga wa Yehova na wa Gideoni!’ Wanaume wake 300 wakafanya vivyo hivyo. Wamidiani waliogopa na kukimbia ovyoovyo. Kukawa na vurugu, nao wakaanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe. Kwa mara nyingine tena, Yehova aliwasaidia Waisraeli kuwashinda maadui zao.

Askari wa Midiani wakiwa wamejaa woga

“Ili nguvu zinazopita zile za kawaida ziwe za Mungu na si kutoka kwetu.”​—2 Wakorintho 4:7

Maswali: Yehova alimthibitishiaje Gideoni kwamba alikuwa amemchagua? Kwa nini jeshi la Gideoni lilikuwa na wanaume 300 tu?

Waamuzi 6:1–16; 6:36–7:25; 8:28

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki