Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 43 uku. 104
  • Dhambi ya Mfalme Daudi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Dhambi ya Mfalme Daudi
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Matata Katika Nyumba ya Daudi
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Tegemea Roho ya Mungu Unaposhughulika na Mabadiliko ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Sababu Inayofanya Watu Watende Mabaya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Ungamo Liletalo Ponyo la Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 43 uku. 104
Nabii Nathani akimshauri Mfalme Daudi

SOMO LA 43

Dhambi ya Mfalme Daudi

Sauli alipokufa, Daudi akawa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka 30. Baada ya kuwa mfalme kwa miaka kadhaa, usiku mmoja akiwa juu ya paa la nyumba ya mfalme alimwona mwanamke mrembo. Daudi akaambiwa kwamba mwanamke huyo anaitwa Bath-sheba na kwamba alikuwa mke wa mwanajeshi aliyeitwa Uria. Daudi akaagiza Bath-sheba aletwe kwenye nyumba yake ya kifalme. Akalala naye, na Bath-sheba akawa mja-mzito. Daudi alijaribu kuficha kile alichokuwa amefanya. Alimwambia mkuu wa jeshi lake amweke Uria kwenye mstari wa mbele wa vita kisha waondoke na kumwacha peke yake. Uria alipouawa vitani, Daudi akamwoa Bath-sheba.

Mfalme Daudi akitoa sala ya kuomba msamaha

Lakini Yehova aliona mambo yote mabaya yaliyotukia. Angefanya nini? Yehova alimtuma nabii Nathani aende kwa Daudi. Nathani akamwambia hivi: ‘Mwanamume fulani tajiri alikuwa na kondoo wengi, na mwanamume maskini alikuwa na mwana-kondoo mmoja mdogo ambaye alimpenda sana. Yule tajiri akamchukua mwana-kondoo wa yule mwanamume maskini.’ Daudi akakasirika na kusema: ‘Huyo mwanamume tajiri anastahili kufa!’ Ndipo Nathani akamwambia Daudi: ‘Wewe mwenyewe ndiye yule tajiri!’ Daudi akahuzunika sana, akamwambia Nathani waziwazi hivi: ‘Nimemtendea Yehova dhambi.’ Dhambi hiyo ilimletea Daudi na familia yake matatizo mengi sana. Yehova alimwadhibu Daudi, lakini akamwacha aendelee kuwa hai kwa sababu alikuwa mnyoofu na mnyenyekevu.

Daudi alitaka kumjengea Yehova hekalu, lakini Yehova akamchagua Sulemani mwana wa Daudi alijenge. Daudi alianza kukusanya vitu kwa ajili ya Sulemani na kusema: ‘Hekalu la Yehova linapaswa kuwa lenye utukufu. Sulemani ni mchanga, lakini nitamfanyia matayarisho.’ Daudi alichangia pesa nyingi kwa ajili ya kazi hiyo ya ujenzi. Akatafuta wafanyakazi wenye ustadi. Akakusanya dhahabu na fedha, na akaleta mierezi kutoka Tiro na Sidoni. Alipokaribia kufa, Daudi akampa Sulemani ramani ya ujenzi wa hekalu. Akamwambia hivi: ‘Yehova aliniagiza niandike mambo haya yote kwa ajili yako. Yehova atakusaidia. Usiogope. Uwe mwenye nguvu na uanze kazi.’

Daudi akizungumzia ramani ya ujenzi na kijana Sulemani

“Anayefunika makosa yake hatafanikiwa, lakini yeyote anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.”—Methali 28:13

Maswali: Daudi alifanya dhambi gani? Daudi alifanya nini ili kumsaidia mwana wake Sulemani?

2 Samweli 5:3, 4, 10; 7:1-16; 8:1-14; 11:1–12:14; 1 Mambo ya Nyakati 22:1-19; 28:11-21; Zaburi 51:1-19

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki