Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 2/1 kur. 3-4
  • Sababu Inayofanya Watu Watende Mabaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Inayofanya Watu Watende Mabaya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Habari Zinazolingana
  • Ungamo Liletalo Ponyo la Kiroho
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Dhambi ya Mfalme Daudi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Matata Katika Nyumba ya Daudi
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Tegemea Roho ya Mungu Unaposhughulika na Mabadiliko ya Maisha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 2/1 kur. 3-4

Neno la Mungu Li Hai

Sababu Inayofanya Watu Watende Mabaya

HUYU mwanamume aliye hapa mbele akifanya pigano karibu na ukuta ni Uria. Mfalme Daudi wa Israeli alikuwa amemwandikia barua Yoabu, jemadari wa jeshi lake, akamwambia: “Mwekeni Uria mbele ya watu penye vita vikali, kisha ondokeni, mmwache, ili apigwe, akafe.”—⁠2 Samweli 11:15.

Uria alikuwa mwanamume mwema, mshikamanifu. Basi, kwa sababu gani Daudi, ambaye pia alikuwa mtumishi wa Yehova, aagize kwa makusudi Uria auawe?

Linaloweza kutusaidia tufahamu jambo hilo ni kusoma mistari inayofuata ya Biblia: “Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”​—⁠Yakobo 1:​13-15.

Lakini huenda ukauliza, ni kwa njia gani habari hizi zinatusaidia tufahamu sababu iliyomfanya Daudi aagize Uria auawe? Ili kupata jibu tunahitaji kuchunguza hali zilizosababisha Daudi atake Uria auawe.

Siku moja, Uria alipokuwa ameenda zake, Daudi alikuwa akitazama akiwa kwenye dari ya nyumba yake kisha akamwona Bath-sheba mke mrembo wa Uria akioga. Daudi alifanya nini? Aliendelea kutazama. Kwa kufanya hivyo aliacha tamaa ya kufanya ngono na Bath-sheba ikue ndani ya moyo wake. Si Mungu aliyekuwa akimjaribu au kumshawishi Daudi. Hapana, Daudi alivutwa na kushawishwa na tamaa yake mwenyewe.

Mwishowe, tamaa mbaya iliyokuwa ndani ya Daudi ikawa yenye nguvu sana hata akaagiza Bath-sheba aletwe kwenye jumba la kifalme lake. Humo akafanya ngono naye. Baadaye, kwa sababu Bath-sheba alikuwa amechukua mimba na Daudi alishindwa kuficha uzinzi huo, alipanga Uria auawe katika pigano.

Ni kweli kwamba dhambi ya Daudi haikumwongoza apoteze milele upendeleo wa Mungu na kupokea hukumu Yake ya kifo. Hiyo ni kwa sababu Daudi alitubu kwa weupe wa moyo, na Yehova akamwonyesha rehema. (Zaburi 51:​1-14) Hata hivyo, tukio hilo linatusaidia kufahamu kwamba mara nyingi watu wanatenda mabaya kwa sababu wanaweka tamaa mbaya katika moyo wao. Kwa hiyo imetupasa sisi tujifunze kutokana na lililompata Daudi kuwa tunaepuka hali, na pia utendaji na tafrija, ambazo zinachochea “hamu ya ngono.”—⁠Wakolosai 3:5, NW; 1 Wathesalonike 4:3-5, UV.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki