Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 47 uku. 114-uku. 115 fu. 3
  • Yehova Amwimarisha Eliya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yehova Amwimarisha Eliya
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Igeni Imani Yao
  • Alifarijiwa na Mungu Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je, wakati fulani unajihisi mpweke na kuogopa?
    Wafundishe Watoto Wako
  • Je, Utakuwa Mwaminifu Kama Eliya?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 47 uku. 114-uku. 115 fu. 3
Eliya akisimama nje ya pango kwenye Mlima Horebu na kumsikiliza malaika wa Mungu

SOMO LA 47

Yehova Amwimarisha Eliya

Yezebeli aliposikia kilichowapata manabii wa Baali, alikasirika sana. Akamtumia Eliya ujumbe unaosema hivi: ‘Kesho, utakuwa umekufa kama tu hao manabii wa Baali.’ Eliya akaogopa sana na kukimbilia jangwani. Akasali: ‘Yehova, siwezi kuvumilia zaidi. Acha nife.’ Eliya akalala usingizi chini ya mti kwa kuwa alikuwa amechoka.

Malaika akamwamsha Eliya na kumwambia hivi kwa sauti tulivu: ‘Amka ule.’ Eliya akaona mkate wa mviringo uliokuwa juu ya mawe yenye moto na gudulia la maji. Akala na kunywa kisha akalala tena. Malaika akamwamsha tena baadaye na kusema: ‘Kula. Unahitaji nguvu kwa ajili ya safari yako.’ Kwa hiyo, Eliya akala tena. Kisha akasafiri kwa siku 40 mchana na usiku, hadi alipofika kwenye Mlima Horebu. Eliya akaingia ndani ya pango ili alale. Lakini Yehova akazungumza naye. Akamwambia: ‘Unafanya nini hapa, Eliya?’ Eliya akamjibu: ‘Waisraeli wamevunja agano lako. Wamebomoa madhabahu zako na kuua manabii wako. Sasa wanajaribu kuniua mimi pia.’

Yehova akamwambia: ‘Nenda usimame kwenye mlima.’ Kwanza, upepo wenye nguvu ukapita kwenye pango hilo. Kisha, kukawa na tetemeko halafu moto. Mwishowe, Eliya akasikia sauti tulivu, ya chini. Akafunika uso wake kwa koti lake na akasimama nje ya pango hilo. Kisha Yehova akamuuliza kwa nini alikuwa akikimbia. Eliya akasema: ‘Nimebaki peke yangu.’ Lakini Yehova akamwambia: ‘Hujabaki peke yako. Kuna watu wengine 7,000 katika Israeli ambao bado wananiabudu. Nenda umweke rasmi Elisha awe nabii badala yako.’ Mara moja, Eliya akaenda na kufanya kama Yehova alivyomwambia afanye. Je, unafikiri Yehova atakusaidia unapofanya kile ambacho yeye anataka ufanye? Ndiyo, atafanya hivyo. Acheni tujifunze jambo lingine lililotendeka wakati wa ukame.

“Msihangaike kuhusiana na jambo lolote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani, mjulisheni Mungu maombi yenu.”​—Wafilipi 4:6

Maswali: Kwa nini Eliya alikimbia? Yehova alimwambia nini Eliya?

1 Wafalme 19:1-18; Waroma 11:2-4

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki