Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 75 uku. 178-uku. 179 fu. 4
  • Ibilisi Anamjaribu Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ibilisi Anamjaribu Yesu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Tuepuke Vishawishi
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • ‘Mpinge Ibilisi’ Kama Yesu Alivyofanya
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Jifunze Kutokana na Jinsi Yesu Alivyokabiliana na Vishawishi
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Kujifunza Kutokana na Vishawishi vya Yesu
    Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 75 uku. 178-uku. 179 fu. 4
Yesu anakataa kuruka kutoka kwenye sehemu iliyoinuka zaidi hekaluni

SOMO LA 75

TIbilisi Anamjaribu Yesu

Yesu anakataa kubadili mawe yawe mikate

Baada ya Yesu kubatizwa, roho takatifu ilimwongoza aingie nyikani. Hakula kitu chochote kwa siku 40, naye akawa na njaa sana. Kisha Ibilisi akaja kumjaribu Yesu na kumwambia hivi: ‘Ikiwa kweli wewe ni Mwana wa Mungu, yaambie mawe haya yawe mkate.’ Lakini Yesu akajibu kwa kunukuu Maandiko akisema: ‘Imeandikwa kwamba mtu anahitaji mengi zaidi ya chakula ili aendelee kuishi. Anahitaji kusikiliza kila neno ambalo Yehova anasema.’

Kisha, Ibilisi akamjaribu Yesu na kumwambia: ‘Ikiwa kweli wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe kutoka kwenye sehemu ya juu zaidi ya hekalu. Imeandikwa kwamba Mungu atawatuma malaika zake wakubebe mikononi mwao.’ Lakini kwa mara nyingine Yesu akanukuu Maandiko na kusema: ‘Imeandikwa kwamba hupaswi kumjaribu Yehova.’

Yesu anakataa falme zote za ulimwengu ambazo Shetani anataka kumpa

Kisha, Shetani akamwonyesha Yesu falme zote za ulimwengu, utajiri wake, na utukufu wake naye akasema: ‘Nitakupa falme hizi zote na utukufu wake ikiwa utaniabudu mara moja tu.’ Lakini Yesu akajibu hivi: ‘Nenda zako, Shetani! Imeandikwa kwamba unapaswa kumwabudu Yehova peke yake.’

Kisha Ibilisi akaondoka, na malaika wakaja na kumpa Yesu chakula. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Yesu akahubiri habari njema ya Ufalme. Hiyo ndiyo kazi aliyotumwa kufanya duniani. Watu walipenda sana mambo ambayo Yesu aliwafundisha, nao wakamfuata kila mahali alipoenda.

“[Ibilisi] anaposema uwongo, yeye husema kulingana na mwelekeo wake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na ndiye baba ya uwongo.”​—Yohana 8:44

Maswali: Yesu alijaribiwa kwa njia gani tatu? Yesu alimjibuje Ibilisi?

Mathayo 4:1-11; Marko 1:12, 13; Luka 4:1-15; Kumbukumbu la Torati 6:13, 16; 8:3; Yakobo 4:7

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki