Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 103 uku. 238-uku. 239 fu. 2
  • “Ufalme Wako na Uje”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ufalme Wako na Uje”
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Kusudi la Mungu kwa Dunia?
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Kusudi la Mungu kwa Wanadamu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Maisha ya Taabu Yanaanza
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Kusudi la Mungu Kuelekea Dunia Litatimizwa Karibuni
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 103 uku. 238-uku. 239 fu. 2
Watu wazima na watoto wakifurahia maisha katika Paradiso

SOMO LA 103

“Ufalme Wako na Uje”

Yehova anaahidi hivi: ‘Hakutakuwa tena na kilio, maumivu, magonjwa, au kifo. Nitafuta kila chozi kutoka katika macho yao. Mambo yote mabaya ya zamani yatasahauliwa.’

Yehova aliwaweka Adamu na Hawa katika bustani ya Edeni ili waishi kwa furaha na amani. Walipaswa kumwabudu Baba yao wa mbinguni na kuijaza dunia. Adamu na Hawa hawakumtii Yehova, lakini kusudi lake halikubadilika. Katika kitabu hiki tumeona kwamba kila kitu ambacho Mungu ameahidi lazima kitimie. Ufalme wake utaleta baraka nzuri ajabu duniani, kama tu alivyomwahidi Abrahamu.

Watu wazima, watoto, na wanyama-mwitu wakiwa pamoja katika Paradiso

Hivi karibuni, Shetani, roho wake waovu, na watu wote wabaya hawatakuwepo. Kila mtu aliye hai atamwabudu Yehova. Hatutakuwa wagonjwa wala hatutakufa. Badala yake, kila siku tutaamka tukiwa wenye nguvu na wenye furaha kwa sababu tuko hai. Dunia itakuwa paradiso. Kila mtu atakuwa na chakula kizuri na kuishi kwa usalama. Watu watakuwa wenye fadhili, si wakatili au wenye jeuri. Hatutahofu wanyama-mwitu, nao pia hawatatuogopa.

Itakuwa pindi yenye kusisimua sana wakati ambapo Yehova ataanza kuwafufua watu. Tutawakaribisha wale walioishi nyakati za kale kama vile Abeli, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Ruthu, Esta, na Daudi. Watashirikiana nasi kuifanya Dunia iwe paradiso. Siku zote kutakuwa na kazi nyingi zenye kufurahisha.

Yehova anataka uishi katika paradiso. Utapata nafasi ya kujifunza mambo mengi zaidi kumhusu. Acheni kila siku tuendelee kumkaribia Yehova zaidi na zaidi, sasa na milele!

“Unastahili, Ee Yehova Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote.”​—Ufunuo 4:11

Maswali: Ni katika njia zipi Ufalme wa Mungu utabadili maisha duniani? Kati ya watu wote ambao umesoma kuwahusu katika kitabu hiki, ni nani ambaye ungependa kukutana naye katika paradiso?

Ufunuo 21:3, 4; Ayubu 33:25; Methali 2:21, 22; Isaya 11:2-10; 33:24; 65:21; Mathayo 6:9, 10; Yohana 5:28, 29; 17:3

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki